Biashara ya ngono na ushoga vita vikali na rc makonda

Biashara ya ngono na ushoga vita vikali na rc makonda

1
876
0
Thursday, 01 November 2018
Local News

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda ameunda kamati maalum ya watu 17 ili kuhakikisha kuwa watu wanaofanya biashara chafu za ngono wanachukuliwa hatua za kisheria.

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam

Kamati hiyo ambayo imejumuisha watu kutoka bodi ya filamu, Mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA, polisi kutoka kitengo cha kuzuia uhalifu wa mitandao,madaktari na wanasaikolojia.

Makonda amesema kuwa kamati hiyo aliyoiunda itafanya kazi katika makundi manne;

  • Kamati itakayoshughulika na mashoga wanaojitangaza na wasiojitangaza lakini wanajulikana kuwa mashoga.
  • Kamati itakawashughulikia wale wote wanaotengeneza picha au video za ngono ambapo mpaka sasa tayari ana udhibitisho wa taarifa za nyumba 24 ambazo zinashughulika na kazi hiyo.
  • Kundi ambalo litaangazia watu wote wanaotangaza biashara ya ngono kwa njia ya mtandao ya kijamii kama instagram,whatsapp na facebook.
  • Kundi la mwisho ni kundi la watu wanaofanya utapeli kwa njia ya mtandao kwa kutumia majina ya watu wengine vibaya ili kujipatia fedha.

Mkuu huyo wa mkoa wa Dar es salaam amesisitiza pia ifikapo jumatatu tarehe 5 Novemba, kila mtu ahakikishe kuwa hana picha chafu ya ngono katika simu yake kwa sababu zoezi hilo litaanza rasmi siku hiyo.

Aidha nyumba zote zinazofanya biashara ya madanguro na kuchua (massage) wahakikishe kuwa wamesajiliwa na wanatumia wataalamu na kama hawafuati utaratibu basi watajulikana kuwa wanafanya biashara ya ngono.

Makonda ameshukuru pia tangu atoe namba ya simu hapo jana ili watu watoe taarifa juu ya watu wanaojishughulisha na biashara hiyo tayari ana ujumbe 18,972 ambapo wote wanalaani vitendo hivyo.

Hata hivyo Makonda amezionya na kutoa angalizo kwa mashirika ya haki za binadamu kuwa Tanzania ina tamaduni zake na ushoga ni kesi ya jinai kwa mujibu wa kifungu cha 154 ambacho kinasema mtu yeyote ambaye anamuingilia mtu yeyote kinyume cha maumbile au, anamuingilia mnyama kimwili au anamruhusu mwanaume kumuingilia yeye mwanaume au mwanamke kinyume cha maumbile,atakuwa ametenda kosa, na atawajibika kwa adhabu ya kifungo cha maisha na wakati mwingine kifungo kisichopungua miaka thelathini .

“Tayari nimepokea majina kadhaa ya watu maarufu katika biashara hiyo na kuna wengine ambao wameeleza kuwa walianza bila kutaka na wanataka kuacha ushoga,”

na kuna ambao wanafanya biashara hiyo kwa hiari na kuna wale wanaowekewa vilevi na kufanyishwa biashara hiyo ambao wote watashughulikiwa”, Makonda aeleza.

Na mwisho amesisitiza kuwa mapambano haya dhidi ya ushoga na biashara ya ngono sio yake peke yake bali ni ya watu wote .

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *