BOKO HARAM YAFANYA SHAMBULIZI KASKAZINI MASHARIKI MWA NIGERIA

BOKO HARAM YAFANYA SHAMBULIZI KASKAZINI MASHARIKI MWA NIGERIA

Like
206
0
Monday, 02 February 2015
Global News

shambulio la wanamgambo wa itikadi kali wa Boko Haram katika mji wa kaskazini mashariki ya Nigeria-Maiduguri,limeangamiza maisha ya watu wasiopungua wanane.

Mashahidi wanasema Boko Haram wamepambana na vikosi vya serikali vinavyosaidiwa na raia katika mapigano ambayo yalianza saa tisa za alfajiri ya leo.

Vikosi vya serikali vinasaidiwa na jeshi la nchi kavu, na lile la wanaanga. Katika siku za hivi karibuni Boko Haram wameeneza hujuma zao hadi katika nchi jirani ya Cameroon.

 

Comments are closed.