Brexit ilivyomuondoa madarakani Theresa May

Brexit ilivyomuondoa madarakani Theresa May

Like
427
0
Saturday, 25 May 2019
Global News

Waziri mkuu wa pili mwanamke Uingereza, kama ilivyo kwa wa kwanza, mwishowe ameondolewa madarakani kutokana na mvutano wa ndani ya chama cha Conservative kuhusu Ulaya.

 

Lakini huenda Theresa May asiwe kama Margaret Thatcher katika orodha ya viongozi walioacha alama ya kudumu katika nchi yao.

Angalau sio kwa namna ambavyo angetamani wakati alipoingia Downing Street mnamo Julai 2016.

Maazimio aliyokuwa nayo – kufikia maenoe yaliosahauliwa katika taifa hilo, au kusahihisha masuala nyeti ya dhulma katika jamii ya Uingereza – yaligubikwa kwa neno moja: Brexit.

Takriban muda wa miaka mitatu aliyohudumu yote yalifafanuliwa kwa uamuzi wa kujiondoa katika Umoja wa Ulaya na jitihada zake kupata ufumbuzi wa matokeo ya kura ya maoni iliyoitishwa na mtangulizi wake David Cameron.

Hata wakosoaji wake wakali walishangazwaa kwa uwezo wake wa kuhimili adhabu na aibu iliyofuata wimbi baada ya wimbi kutoka Brussels na Westminster.

Mpambano wa kuwasilisha Brexit

Kujiuzulu kwa mawaziri na wabunge wa upinzani ambayo yote yangebaini mwisho wa uhusiano wa kawaida kwa waziri mkuu yalioonekana kutomtetelesha.

Aliendelea ni kana kwamba hata hatambui kizaa zaa kinachomzungka na kuwamabia wabunge “hakuna kilichobadilika” na kuahidi kutekeleza “wanachotaka” raia wa Uingereza, hata wakati nguvu zake bungeni na udhibiti wa chama chake kilichoshuka umaarufu ukiendelea kupungua.

Huenda taswira ingekuwa tofuati iwapo angeshinda katika uchaguzi mkuu aliouitisha mnamo 2017.

Lakini badala ya kurudi Downing Street na jukumu kubwa mikononi, kama alivyotarajia, alipoteza uwingi katika bunge la wawakilishi na imbidi ategemee uungwaji mkono wa kutoka chama cha Ireland kaskazini Democratic Unionist Party.

Hakupoa kidonda hichi, na kumekuwana hisia kwamba wabunge wake wengi walikuwa wamemaucha aendele kuhdumu mpaka pale atakapofanikiwa kuwasilisha mpango wa Uingereza kujitoa katika Umoja wa Ulaya kabla ya kumtema baada ya kupata mpango mbadala unaovutia.

Kwa wakati mmoja, ilibidi aahidi atajiuzulu kabla ya uchaguzi ujao wa 2022 wakati akijizatiit kuponea kura ya kutokuwana imani naye iliyooidhinishwa na wabunge wake mwenyewe.

Na baada ya kutengwa na wabunge wengi kwa kuwalauamu kwa mkwamo wa Brexit, alilazimika hatimaye kukubali kwamba chama chake, cha Conservative hakikumtaka aendelee kuhudumu tena.

Ajitolea mara ya mwisho

Amejitolea kuondoka kama hatua ya mwisho kwa wakosoaji wakena kuwamabi kwamba atajiuzulu iwapo wtaapiga kura kukubali mpango wa kujitoa katika Umoja wa Ulaya aliyoupigia upatu huko Brussels.

Januari 2019, bunge lilipinga mpango huo kwa uwingi mkubwa kuwahi kufanyika dhiid ya serikali Uingereza katika historia.

May amejaribu tena mara mbili kupata ridhaa ya bunge, kwa kukarabati mpango huo na alishindwa tena mara zote.

 

Watu wanaounga mkono kusalia walidhani kwamba makubaliano hayo ni makali mno, huku wa Conservative wakisema haujatimiza Uingereza kujitoa kikamilifu kutoka Umoja wa Ulaya.

Katika jitiahada ya kujadiliana makubaliano ya Brexit ambayo yanaweza kupita katika bunge la wawakilishi alishauriana na kiongozi wa chama cha Leba Jeremy Corbyn.

Lakini mazungumzo ya wiki sita pasi kufikiwa makubaliano , matokeo ambayo wabunge wengi wa Conservative wanasema yalitabirika na ni ya kuvunja moyo.

Izara nyingine ilifuata wakati alilazimika kukubali Uingereza kushiriki katika uchaguzi kwenye Umoja wa Ulaya – jambao ambalo hapo awali alisema halitokubalika.

Kufikia hatua hii wabunge waliacha kumsikiliza, kwa kufikia uamuzi kwamba May ni kizuizi kwa Brexit wanayoitamani- au ya aina yoyote ile.

Hatimaye May alilazimika kukubali kwamba hawezi kuendelea “katika kazi anayeoipenda” na muda wake huko Downing Street sasa umemalizika.

Sauti yake ilitetereka na alikuwa mwingi wa hisia alipomaliza hotuba yake akisema: “Nitaondoka katika wadhifa huu hivi karibuni lakini imekuwa heshima kubwa maihsani mwangu kuhudumu.

Atajiuzulu kama kiongozi wa chama hicho Juni 7 na uteuzi wa waziri mkuu mpya unatarajiwa kuanza wiki inayoafuata baada ya hatua hiyo.

 

cc;BBCswahili

 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *