Local News

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA AZINDUA JARIDA LA KIMATAIFA LA FIRST
Local News

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA amezindua jarida la Kimataifa la FIRST ambalo limesheheni taarifa za kuitangaza Tanzania kwa wadau wa nchi mbalimbali duniani huku likielezea hatua mbalimbali za ustawi kwa miaka 50 tangu nchi ipate uhuru. Uzindusi huo umefanyika Ofisi za Ubalozi wa Tanzania jijini London, Uingereza ambako pia Waziri Mkuu amekabidhiwa nakala ya kwanza ya toleo la sasa ambayo imewekwa kwenye jalada. Akizungumza katika uzinduzi huo, Waziri Mkuu amebainisha kuwa, Serikali ya Tanzania imepata fursa ya kujinadi kwa watu maarufu...

Like
299
0
Thursday, 23 October 2014
WATANZANIA WASHAURIWA KUTOTEGEMEA ZAIDI UGUNDUZI WA MAFUTA NA GESI
Local News

WATANZANIA wameshauriwa kutotegemea zaidi ugunduzi wa mafuta na gesi kuwa ndio njia pekee ya kutatua matatizo ya kiuchumi nchini. Akizungumza na wadau mbalimbali jijini Dar es salaam kwenye kongamano la kufunga maonesho ya tatu ya mafuta na gesi asilia Naibu Waziri wa Nishati na Madini mheshimiwa STEVEN MASELE amesema kuwa wananchi wanatakiwa kutumia fursa hiyo kama njia moja wapo ya kuinua vyanzo vingine vya uchumi  MASELE Aidha Mheshimiwa MASELE amebainisha kuwa Serikali imeandaa mkakati wa kufungua mfuko utakaotumika kuifadhi mapato...

Like
280
0
Thursday, 23 October 2014
KAMATI YA HESABU ZA SERIKALI ZA MITAA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO MWANZA NA IRINGA
Local News

KAMATI ya Hesabu za Serikali za mitaa inatarajia kwenda kukagua miradi ya maendeleo pamoja na kukagua mapato na matumizi katika Halmashauri za mikoa ya Mwanza na Iringa. Hayo yamebainishwa na mwenyekiti wa Kamati hiyo RAJAB MBARUK MOHAMED ambapo amesema Kamati itaondoka leo kwa kuwa ripoti ya CAG inaonyesha kuwa Mwanza ndiyo ilifanya vibaya zaidi kuliko zote…. Hata hivyo amesema, kuna fedha zaidi ya bilioni mia tatu zilizotolewa na wafadhiri kwa ajili ya Halmashauri hazikutumika. MOHAMED...

Like
274
0
Thursday, 23 October 2014
TANESCO PAMOJA NA REA WAPELEKA WATAALAMU WILAYA YA MKULANGA
Local News

SHIRIKA la umeme nchini Tanesco kwa kushirikiana na wakala wa umeme vijijini -REA- wamefanikiwa kupeleka wataalamu wakutoa elimu ya matumizi sahihi na salama ya umeme katika vijiji vyote vya wilaya ya mkuranga ikiwa ni utekelezaji wa ahadi waliyoitoa kupitia kwa naibu waziri wa fedha ADAMU MALIMA. Akizungumza na EFM Ofisini kwake jijini Dar es salaam meneja wa Tanesco kanda ya Pwani na Dar es salaam MAHENDE MUGAYA amesema kuwa wataalamu hao watatoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa kutumia...

Like
500
0
Wednesday, 22 October 2014
MCT YAZINDUA TUZO ZA UMAHIRI ZA UANDISHI WA HABARI
Global News

 BARAZA la habari nchini-MCT kwakushirikiana na Kamati ya maandalizi ya tuzo za Umahiri za uandishi wa habari Tanzania-EJAT, leo imezindua rasmi tuzo hizo ikiwa ni mara ya sita tangu kuanzishwa kwake. Akizungumza na wandishi wa habari Jijini Dar es salaam, kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya EJAT, Meneja udhibiti na viwango wa MCT, Pili Mtambalike amesema tuzo za mwaka huu zimeongezewa mambo mapya mawili nakufanya jumla ya makundi ya kushindaniwa kuwa 21 kutoka 19. PICHA NI BAADHI...

Like
431
0
Tuesday, 21 October 2014
VIKAO VYA KAMATI YA BUNGE VIMEENDELEA LEO JIJINI DAR
Local News

VIKAO vya kamati za Bunge vimeendelea leo jijini Dar es salaam ikiwa ni siku ya pili ambapo ripoti za Serikali Kuu na Mashirika ya Umma zimewasilishwa zikifatiwa na taarifa ya Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka 2012-2013 Katika Kamati ya Hesabu za Serikali na Mashirika ya Umma-PAC. Akisoma Ripoti ya CAG, mbele ya mwenyekiti wa kamati hiyo Zitto Kabwe, Msaidizi Mkaguzi Mkuu Nestory Karia amesema ofisi yake imebaini mapungufu mengi ya fedha katika baadhi...

Like
371
0
Tuesday, 21 October 2014
IMANI POTOFU NI KIKWAZO KWENYE UTOAJI WA CHANJO
Local News

IMEELEZWA KUWA, Imani Potofu dhidi ya Chanjo za Surua na Rubella zinazoendelea kutolewa kote nchini, zimekuwa kikwazo katika kufanikisha kampeni hiyo yenye lengo la kupunguza ongezeko la magonjwa ya milipuko kwa watoto wenye umri wa kuanzia miezi tisa hadi miaka 15. Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya Ilala RAYMOND MUSHI wakati wa uzinduzi wa chanjo ya Surua na Rubella… Naye Mgeni rasmi katika uzinduzi huo, bwana REGINALD MENGI amesema hilo. Kwa upande wake mratibu wa chanjo mkoa wa Dar...

Like
375
0
Tuesday, 21 October 2014
SIMU ZA MIKONONI, VYOMBO VYA HABARI KUTUMIKA KUTOA TAARIFA ZA AFYA
Local News

CHAMA Cha Wataalam wa Habari za afya Afrika-AHILA kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii wameandaa mikakati ya kusambaza taarifa muhimu za afya kwa wananchi kwa kutumia mitandao ya habari ikiwemo simu za mikononi Akizungumza na wadau mbalimbali jijini Dar es salaam katika uzinduzi wa mkutano wa kumi na nne wa wataalam wa habari za afya Afrika, Makamu wa Rais Dokta AHMED BILALI amesema kuwa taarifa za afya kutoka kwa wataalam mbalimbali wa afya nchini zitawafikia wananchi...

Like
266
0
Tuesday, 21 October 2014
EBOLA YATINGA TANZANIA!!!
Local News

  MWILI wa mtu mmoja anayesadikiwa kuwa na ugonjwa wa Ebola Wilayani Sengerema Mkoani mwanza umezikwa jana kwa tahadhari kubwa na wataalamu wa afya. Mgonjwa huyo anayedaiwa kufariki kwa Ebola Salome Richard mwenye umri wa miaka 17, alifikishwa katika hospitali ya Sengerema siku ya Ijumaa wiki iliyopita nakufariki siku hiyo hiyo. Kwa mujibu wa muunguzi aliyempokea mgonjwa huyo SUZANA JONATHAN ambaye pia bado amewekwa chini ya uangalizi maalumu, mgonjwa huyo alifika hospitalini hapo akiwa anatokwa damu sehemu mbalimbali za wazi...

Like
415
0
Monday, 20 October 2014
VIJANA WATAKIWA KUMUENZI BABA WA TAIFA KWA KUDUMISHA MUUNGANO
Local News

VIJANA wa Vyuo vya Elimu ya Juu na wametakiwa kuachana na fikra potofu za kudhani kuwa Serikali tatu ndio Suluhisho la Kero ya Muungano badala yake wametakiwa kudumisha Muungano kwa Kumuenzi Baba wa Taifa Hayati mwalimu JULIUS NYERERE. Hayo yamebainishwa Jijini Dar es salaam na Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi-CCM Bara PHILIP MANGULA wakati akizungumza katika mkutano wa Vijana Wanafunzi wa vyuo Vikuu. Kwa upande wake Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama hicho NAPE NNAUYE amevibeza Vyama vya...

Like
263
0
Monday, 20 October 2014
CHADEMA YAKUTANA KUJADILI MCHAKATO WA KATIBA MPYA
Local News

KAMATI kuu ya chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA imekutana katika kikao chake cha kawaida kujadili pamoja na mambo mengine mchakato wa katiba mpya. Kamati Kuu imepata taarifa ya kina juu ya mchakato ulivyoendeshwa katika hatua mbalimbali wakati wa kutungwa kwa sheria ya katiba na marekebisho yake na baadaye, sheria ya kura ya maoni  TUNDU LISSU Naye Katibu Mkuu wa Chama hicho, DR WILLBROD SLAA amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura katika uchaguzi wa serikali...

Like
264
0
Friday, 17 October 2014