Local News

MAHAKAMA KUU LEO KUSIKILIZA KESI YA IPTL NA PAP DHIDI YA DAVID KAFULILA
Local News

MAHAKAMA kuu ya Tanzania leo kwa mara ya pili itasikiliza kesi namba 131 iliyofunguliwa na Singasinga, SETHI, Kampuni za IPTL na PAP dhidi ya Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila.                   Katika kesi hiyo Kafulila anadaiwa shilingi bilioni 310 na Kampuni hizo kwa madai ya kuzichafua kwakuziita za kifisadi na kwamba ziepora fedha kiasi cha bilioni 200 kwenye akaunti ya Escrow kinyume cha taratibu Katika kesi ya kwanza, Mheshimiwa Kafulila kupitia kwa...

Like
397
0
Thursday, 30 October 2014
WANAWAKE TANGA WATAKIWA KUJITOKEZA NA KUCHANGAMKIA FURSA
Local News

WANAWAKE wajasiriamali mkoani Tanga wametakiwa kujitokeza na kuchangamkia fursa zitakazotolewa na kampeni ya mwanamke na uchumi inayotarajiwa kutolewa mwanzoni mwa mwezi ujao mkoani Tanga ambapo zaidi ya wanawake 300 watanufaika na mafunzo hayo yanayotolewa na kampuni ya Angels Moment ya jijini Dar Es Salaam. Mkuu wa wilaya ya Tanga Mheshimiwa Halima Dendego amesema fursa zitakazotolewa ni fahari kwa wanawake na wajasiriamali wa mkoa huo kwani elimu inahitajika sana wakati huu wa ushindani wa biashara.   Mkuu huyo wa wilaya amewaomba...

Like
273
0
Wednesday, 29 October 2014
BAN KI MOON KUTEMBELEA KAMBI YA WAKIMBIZI KENYA
Local News

KATIBU MKUU wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon anatembelea kambi ya wakimbizi ya Daadab, nchini Kenya. Hii ni mara ya kwanza kwa kingozi huyo mkubwa katika Umoja wa Mataifa kutembelea kambi hiyo kubwa ya wakimbizi. Ban Ki Moon anatarajiwa kutathmini hali ya msongamano katika kambi hiyo na hali ya usalama ambayo imekuwa ikizorota mara kwa mara. Aidha ripoti zinasema, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ataidhinisha pia kuondoka kwa baadhi wa wakimbizi wa kisomali waliojitolea kurudi nyumbani.    ...

Like
249
0
Wednesday, 29 October 2014
RAIS WA ZAMBIA MICHAEL SATTA AMEFARIKI DUNIA HUKO LONDON
Local News

RAIS wa Zambia Michal Satta amefariki akiwa London, Uingereza ambako alikuwa akitibiwa ugonjwa ambao bado haujawekwa wazi. Huyu ni Rais wa Pili wa nchi hiyo kufariki akiwa madarakani baada ya Rais Levy Mwanawasa naye kufariki dunia akiwa madarakani miaka kadhaa iliyopita. Kulikuwa na uvumi kuwa Sata alikuwa mgonjwa sana na hajaonekana hadharani tangu aliporejea kutoka katika mkutano wa baraza kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York mwezi uliopita, ambako alishindwa kutoa hotuba aliyopangiwa kuitoa. Alisafiri kwa njia ya ndege...

Like
628
0
Wednesday, 29 October 2014
JESHI LA POLISI LAWATAKA WANANCHI DAR KUTOSAFIRISHA FEDHA KIHOLELA
Local News

JESHI la Polisi kanda Maalum Dar es salaam limewataka wananchi, Taasisi na wafanyabiashara kuacha tabia ya kusafirisha fedha kiholela katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam ili kuepu matatizo ya kuporwa fedha ikiwa ni pamoja na kuhatarisha maisha yao.   Akizungumza na Waandishi wa Habari Kamishna wa Polisi Kanda Maalum Dar es salaam SULEIMAN KOVA amesema hali hiyo inatokana na kuongezeka kwa matukio mbalimbali ya uporaji wa fedha.     Katika hatua nyingine Kamishna Kova amewataka wananchi kuwa...

Like
207
0
Wednesday, 29 October 2014
THRDC YAKUTANA NA JESHI LA POLISI NA KUWEKA MIKAKATI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU
Local News

Katika kuelekea kipindi cha Uchaguzi Mkuu wa mwakani Taasisi ya kutetea haki za binadamu nchini,THRDC wamekutana na Jeshi la Polisi kwa lengo la kutengeneza na kuboresha Mikakati madhubuti ya kufanikisha Uchaguzi huo kuwa wa Huru, Haki na Utulivu.   Akizungumza na Waandishi wa Habari katika Mkutano huo jijini Dar es salaam,Makamu Mkuu wa Jeshi la polisi ABRAHAM KANIKI amesema watahakikisha wanashirikiana vyema na wadau hao ili kuhakikisha madhara hayatokei kwa...

Like
225
0
Tuesday, 28 October 2014
EBOLA: CUBA YATOA MADAKTARI 75 NA WAUGUZI KUMI
Local News

Nchi ya Cuba imejitolea Madaktari 75 na wauguzi 10 kwenda kusaidia nchi zilizoathirika na maradhi ya ugonjwa wa Ebola Afrika. Akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es salaam Balozi wa Cuba nchini Tanzania GEORGE LOPEZ amesema katika kukuza Umoja na Ushirikiano kati ya nchi ya Cuba na Afrika,wameamua kujitolea madaktari hao kusaidia kutoa hudumaza Matibabu katika nchi za Sierion,Liberia. Balozi LOPEZ amesema nchi yake itazidi kuisadia Afrika hasa katika sekta ya afya na elimu....

Like
234
0
Tuesday, 28 October 2014
MADEREVA WA BODABODA WAIOMBA SERIKALI KUWATENGEA MAENEO MAALUMU
Local News

MADEREVA wa Pikipiki maarufu Bodaboda, wameilalamikia Serikali kwa kutowatengea maeneo maalumu ya kupaki pikipiki zao katika kituo kipya cha mabasi cha Ubungo kilichopo Kata ya Sinza C. Wakizungumza na Efm Jijini Dar es salaam Madereva hao wamesema kuwa ujio wa kituo hicho imekuwa ni kero kwani hawana sehemu maalumu ya kupaki na wamekuwa wakiondolewa na vijana wa Ulinzi Shirikishi na kutozwa pesa isio kuwa na kiwango na watu wasiojulikana. Wamebainisha kuwa inapaswa Serikali iwatambue na kuwajali kuwa nao wana mchango...

Like
258
0
Monday, 27 October 2014
BOKO HARAM LATEKA NYARA WATOTO
Local News

WATOTO 30 wametekwa nyara na watu wanaodhaniwa kuwa wapiganaji wa Boko Haram. Watoto hao wametekwa nyara kaskazini mashariki mwa Nigeria. Tukio hili linakuja siku chache baada ya kundi hilo kuwateka wanawake na wasichana kaskazini mashariki mwa nchi hiyo. Hadi sasa wasichana wa shule 200 waliotekwa na wanamgambo hao miezi tisa iliyopita bado hawajulikani walipo....

Like
272
0
Monday, 27 October 2014
NEC KUTUMIA TEKNOLOJIA MPYA KWENYE MABORESHO YA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA
Local News

KUFUATIA Tume ya Taifa ya Uchaguzi -NEC-kutangaza kuanza kwa Maboresho ya Daftari la Kudumu la Wapiga kura kwa Kutumia Tekinolojia mpya, Mbunge wa Mchinga kwa Tiketi ya Chama Cha Mapinduzi -CCM SAID MTANDA amesisitizia Tume kuzingatia vigezo sahihi katika maboresho ya daftari hilo. Akizungumza na EFM kwa njia ya simu amesema umuhimu wa kuboresha Daftari hilo haupo tu katika kuongeza idadi ya wapiga kura bali pia kuondoa watu ambao wamepoteza sifa za kupiga kura kama waliofariki na watu ambao wanatumikia...

Like
286
0
Monday, 27 October 2014
TANZANIA KUUKABILI UMASIKINI VIJIJINI
Local News

WAKATI Taarifa ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa inaonyesha ongezeko la watu wanaoishi katika umaskini  Kusini mwa Jangwa la Sahara Afrika, Tanzania imetaka utekelezaji wa Malengo Mapya ya Maendeleo Endelevu baada ya mwaka 2015 ujielekeze katika kuukabili Umasikini wa Vijijini. Muwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi TUVAKO MANONGI, ameeleza hayo wakati akichangia majadiliano ya Taarifa ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu utekelezaji wa mwongo wa Pili wa utokomezaji Umaskini mwaka – 2008-2017. Katika...

Like
242
0
Thursday, 23 October 2014