Global News

WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA UJERUMANI AWAALIKA MAWAZIRI WENZAKE BERLIN KUJADILI MAKUBALIANO YA AMANI UKRAINE
Global News

WAZIRI wa Mambo ya  Nje wa Ujerumani  Frank – Walter Steinmeier  amewaalika  Mawaziri  wenzake   kutoka  Urusi, Ukraine na  Ufaransa  mjini  Berlin  siku  ya  Jumatatu  kujadili utekelezaji  wa makubaliano  ya  amani  yaliyofikiwa  mjini  Minsk  kuhusu  mashariki mwa  Ukraine, nchini  Belarus Februari mwaka  huu. Mzozo  kati ya waasi wanaoungwa  mkono  na  Urusi  na  Majeshi ya  Serikali  ya  Ukraine  mashariki mwa nchi hiyo umesababisha watu elfu sita kupoteza  maisha. Viongozi  wa ...

Like
186
0
Friday, 10 April 2015
WAZIRI MKUU WA UGIRIKI AWASILI MOSCOW KUFANYA MAZUNGUMZO MAALUM
Global News

WAZIRI Mkuu wa Ugiriki, Alexis Tsipras, amewasili mjini Moscow kukutana rais wa Urusi Vladimir Putin kwa mazungumzo maalum. Ugiriki inasema kuwa mazungumzo yao yatajadili uhusiano kati ya muungano wa bara la Ulaya na Urusi. Uhusiano huo ulidorora kwa kiasi kikubwa katika siku za hivi karibuni kufuatia mzozo wa Ukraine. Wachanganuzi wanasema kuwa Ugiriki inapania kuboresha uhusiano na Moscow hasa ikiwa uhusiano wao na wadeni wao bara Ulaya wa kuikopesha pesa ukishindikana ambapo kesho nchi hiyo inatakiwa kulipa deni la dola...

Like
186
0
Wednesday, 08 April 2015
UGANDA: WATU KADHAA WASHIKILIWA KUFUATIA MAUAJI YA MWENDESHA MASHTAKA JOAN KAGEZI
Global News

UGANDA inasema imekamata watu kadhaa kuhusiana na mauaji ya mwendesha mashtaka Joan Kagezi yaliyotokea wiki iliyopita. Mwendesha mashtaka huyo aliuawa na watu waliokuwa na bunduki wakitumia pikipiki na polisi kuanza uchunguzi kuhusiana na mauaji hayo. Kutokana na matukio ya kigaidi katika nchi jirani ya Kenya, polisi Nchini Uganda wamekuwa wakichukua tahadhari dhidi ya matukio yoyote...

Like
241
0
Wednesday, 08 April 2015
MAREKANI: AFISA WA POLISI AHUKUMIWA KWA MAUAJI YA MTU MWEUSI
Global News

WAKUU katika jimbo la South Carolina nchini Marekani wamemhukumu Afisa mmoja wa polisi mweupe, kwa kosa la mauaji. Mtuhumiwa huyo anadaiwa kumpiga risasi raia mmoja mweusi na kumuuwa. Mkanda wa video unaonesha mtu mmoja, WALTER SCOTT, akipigwa risasi alipokuwa akimkimbia Afisa huyo.  ...

Like
233
0
Wednesday, 08 April 2015
KENYA: WANANCHI WAANDAMANA KUDAI USALAMA ZAIDI
Global News

WAKENYA  wameandamana kudai usalama  zaidi  wa  taifa  hilo kufuatia  mauaji  ya  wiki  iliyopita yaliyofanywa  na  wapiganaji kutoka  Somalia  wa  kundi  la  Al-Shabaab , kabla  ya  kuwasha mishumaa  usiku katika  siku  ya  mwisho  ya  Maombolezi kutokana na  kuuwawa  kwa  watu  148 mjini Garissa. Ndege  za  kivita  za  Kenya  zimeshambulia  maeneo yanayodhibitiwa  na  kundi  hilo  lenye  mafungamano  na  Al-Qaeda Kusini  mwa  Somalia  , lakini  hasira  imekuwa ikiongezeka  kuhusiana  na ...

Like
188
0
Tuesday, 07 April 2015
TONY BLAIR AINGIA KWENYE KAMPENI KWA KUMSHAMBULIA DAVID CAMEROON
Global News

WAZIRI Mkuu wa zamani wa Uingereza,TONY BLAIR ameingia katika kampeni za uchaguzi kwa kumshambulia Waziri Mkuu DAVID CAMERON, kwa ahadi yake ya kufanyika kwa kura ya maoni kuhusu uanachama wa Uingereza katika Umoja wa Ulaya, EU. Bwana BLAIR amesema Bwana CAMERON ametoka nje ya agenda kwa kuahidi kufanyika kura ya maoni na kwamba kujiondoa katika Umoja wa Ulaya kunatishia nafasi ya Uingereza kama taifa kubwa duniani Bwana BLAIR anatarajiwa kusema kuwa kiongozi wa Chama chake cha LABOUR ED MILIBAND ameonyesha...

Like
179
0
Tuesday, 07 April 2015
YEMEN: ZAIDI YA WATU 500 WARIPOTIWA KUUAWA KWENYE MAPIGANO YA HIVI KARIBUNI
Global News

SHIRIKA la Afya Duniani limetoa takwimu zinazosaidia kuelewa wa mgogoro uliopo nchini Yemen. Shirika la WHO limesema Zaidi 500 wameuawa katika mapigano ya wiki za hivi karibuni, na kwamba watu wapatao elfu moja na mia saba wamejeruhiwa katika mapigano hayo. Waasi kama “Houthi” na washirika wao wanapambana na majeshi ya Rais ABD RABBU MANSOUR HADI ambaye anaungwa mkono na jeshi la linaloongozwa na Saudi...

Like
197
0
Tuesday, 07 April 2015
TIMBUKTU: RAIA WA UHOLANZI ALIETEKWA NYARA AKOMBOLEWA
Global News

RAIA wa Uholanzi ambaye aliyetekwa nyara miezi Minne iliyopita na mtandao wa kigaidi wa AQIM, huko  Timbuktu Kaskazini mwa Mali amekombolewa leo katika operesheni za kijeshi za Ufaransa. Wizara ya mambo ya nje ya Ufaransa imesema mateka SJAAK RIJKE, ambaye ametekwa Novemba 25,2011 amekombolewa baada ya kufanyika Operesheni ya Kikosi Maalum cha jeshi la taifa hilo. Taarifa hiyo imesema kuwa operesheni hiyo vilevile imefanikisha kutiwa mbaroni kwa watu wengine...

Like
176
0
Tuesday, 07 April 2015
MAKABURI YAFUKULIWA TIKRIT
Global News

WATAALAMU wa kuchunguza Maiti, wameanza kufukua zaidi ya Makaburi 12 ya halaiki, katika mji wa Tikrit, nchini Iraq. Hatua hiyo imekuja siku kadhaa baada ya Wapiganaji wa Islamic State, kutimuliwa nje ya mji huo. Makaburi hayo yaanaminika kuwa na zaidi ya Maiti Elfu Moja Mia Saba ya Wanajeshi Waislamu wa Kishia, waliouwawa mwezi Juni mwaka jana na Wanamgambo wa...

Like
207
0
Tuesday, 07 April 2015
IRAN YAAFIKI KUPUNGUZA KURUTUBISHA NYUKLIA
Global News

MAKUBALIANO kuhusu muundo wa baadaye wa mpango wa nyuklia wa Iran, yamefikiwa baada ya mazungumzo na mataifa Sita makubwa yaliyokuwa yakifanyika nchini Uswisi. Kwa mujibu wa mkataba huo, Iran itapunguza uwezo wake wa kurutubisha madini ya Urani huku ikiahidiwa kuondolewa vikwazo kwa awamu. Mataifa makubwa ya Dunia na Iran sasa yanalenga kuandika mkataba kabambe ifikapo Juni 30....

Like
185
0
Friday, 03 April 2015
BOTI YA UVUVI YA URUSI YAZAMA, WATU ZAIDI YA HAMSINI WAHOFIWA KUFA MAJI
Global News

BOTI ya uvuvi ya Urusi imezama katika visiwa vya Kamchatka , ikiwa na mabaharia wapatao hamsini na wanne ambao inadhaniwa kuwa wamekufa maji wote. Watu wapatao sitini na watatu wameopolewa ambao nao walikuwa ndani ya boti hiyo ya uvuvi,wengine wamekumbwa na homa ya mapafu na wengine kumi na watano wameripotiwa kuwa hawaonekani. Taarifa za awali zinasema kwamba kabla meli hiyo ya uvuvi haijazama ilikuwa na watu wapatao miamoja na thelathini na mbili ,Wengi wao walikuwa wanatokea maeneo ya Vanuatu, Latvia...

Like
255
0
Thursday, 02 April 2015