Global News

WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA UJERUMANI AONYA KUSAMBAA KWA MZOZO UKRAINE
Global News

WAZIRI wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, FRANK-WALTER STEINMEIER amesema pande zinazohusika katika mzozo wa Ukraine, lazima ziepukane na hatua zozote zinazoweza kupelekea mzozo mpya kusambaa zaidi nchini humo. Aidha, STEINMEIER ametoa wito wa kuendelea kwa mchakato wa mpango wa amani wa Minsk, ambao umesainiwa mwaka uliopita, katika juhudi za kusimamisha mapigano Mashariki mwa Ukraine. STEINMEIER na maafisa wengine waandamizi wanaohusika na mzozo wa Ukraine, wanatarajiwa kukutana mjini Paris, Ufaransa kujadiliana kuhusu hatua za kusitisha mapigano...

Like
185
0
Tuesday, 24 March 2015
UGIRIKI NA UJERUMANI ZASISITIZA NIA YA KUONDOA MVUTANO KATI YA SERIKALI ZAO
Global News

KANSELA wa Ujerumani, ANGELA MERKEL na Waziri Mkuu wa Ugiriki, ALEXIS TSIPRAS wamesisitiza nia yao ya kuondoa mvutano uliopo kati ya serikali zao. Hayo wameyaeleza katika mkutano wao na Waandishi wa Habari uliofanyika mjini Berlin. TSIPRAS amezuru rasmi Ujerumani kwa mara ya kwanza tangu aingie madarakani mwezi Januari mwaka...

Like
178
0
Tuesday, 24 March 2015
ANGELA MERKEL KUKUTANA NA WAZIRI MKUU WA UGIRIKI LEO
Global News

KANSELA wa  Ujerumani  Angela  Merkel  anakutana  leo  na  waziri mkuu  wa  Ugiriki Alexis  Tsipras , ambaye  amemlaumu kansela  kwa kusisitiza  kuhusu  hatua ya  kubana  matumizi  kwa  nchi  yake ambayo  imesababisha  mzozo  wa  kiutu wa umasikini pamoja  na ukosefu  mkubwa  wa  ajira. Viongozi  hao wa  Ugiriki  na  Ujerumani  wanakutana  mjini  Berlin baada  ya  wiki  kadhaa  za hali  ya  wasi  wasi  kuhusiana  na matatizo  ya  upatikanaji  wa  fedha  kwa  Ugiriki , hisia  za  baada ya ...

Like
165
0
Monday, 23 March 2015
KIONGOZI MASHUHURI WA SINGAPORE AFARIKI DUNIA
Global News

KIONGOZI  mashuhuri  wa  Singapore, anayejulikama  kama  baba  wa taifa  hilo , Lee Kuan Yew  amefariki dunia. Serikali  ya  nchi  hiyo imetangaza  hii  leo kwamba  Lee  mwenye  umri  wa  miaka  91 alilazwa  hospitalini  mapema  Februari  akiwa  anaugua  ugonjwa wa  kichomi, na  amekuwa  akipumua  kwa  kutumia  mashine  katika kitengo  cha  wagonjwa  mahututi  tangu wakati  huo. Rais  wa  Marekani  Barack Obama  ametuma salamu  zake  za rambi rambi  na  kumuelezea  Lee  kuwa  mtu  aliyeona ...

Like
249
0
Monday, 23 March 2015
VIDEO: WAZAZI WAWAPITISHIA CHABO WANAFUNZI KWA KUPARAMIA MAGHOROFA
Global News

Wazazi huko india wameparamia ukuta kupitisha majibu ya mitihani kwa watoto wao Watoto katika shule ya Bihar wilaya ya Hajipur wamekuwa wakipata msaada wa kupitishiwa majibu na wazazi wanapokuwa kwenye vyumba vya mitihani. Kwenye mkanda wa video uliorekodiwa na chanzo kimoja cha habari za ndani nchini humo kinaonyesha umati wa wazazi wakiparamia kuta za ghorofa kuwapitishia wanafunzi majibu ya mtihani kwa kutumia madirisha ya jengo hilo Zaidi ya wanafunzi milioni 1.4 wapo katika mitihani ambayo inarajiwa kumalizika march 24 nchini...

Like
354
0
Monday, 23 March 2015
EBOLA: MASHIRIKA YA UTOAJI MISAADA YAONYA HALI NI TETE
Global News

MASHIRIKA ya utoaji misaada yanaonya hali bado ni tete, mwaka mmoja tangu ugonjwa wa maradhi ya Ebola kulipuka Magharibi mwa Afrika. Shirika la Madaktari wasiokuwa na Mipaka- MSF, limesema kuwa mlipuko huo ambao umewauwa zaidi ya watu Elfu Kumi. Shirika limesema namna Mashirika ya Matibabu na watoaji Misaada ya Dharura, yanavyoendesha shughuli za kuwaokoa watu kuwa ni taratibu mno....

Like
177
0
Monday, 23 March 2015
UMOJA WA ULAYA UMEFIKIA MAKUBALIANO KUREFUSHA VIKWAZO VYA UCHUMI DHIDI YA URUSI
Global News

VIONGOZI wa Taifa na Serikali wa nchi za Umoja wa Ulaya wamekubaliana kurefusha vikwazo vya Kiuchumi dhidi ya Urusi hadi Desemba mwaka huu. Katika mkutano wao wa kilele mjini Brussels viongozi hao wa Mataifa 28 wamefungamanisha vikwazo hivyo na kuheshimu makubaliano ya kuweka chini silaha na kurejesha amani Mashariki mwa Ukraine. Hata hivyo Viongozi hao  wamezidi kumshinikiza Rais wa Urus VLADIMIR PUTIN, atumie ushawishi wake kuwatanabahisha Waasi wanaoelemea upande wa Urusi ili kumaliza mzozo wa Mashariki mwa...

Like
181
0
Friday, 20 March 2015
SERIKALI YA MAREKANI YAMTUHUMU NETANYAHU KUKIUKA MPANGO WA AMANI
Global News

MSEMAJI wa Serikali ya Marekani, JOSH EARNEST, amesema Waziri Mkuu wa Israel BENJAMIN NETANYAHU, amekiuka dhamira yake ya awali ya kuundwa kwa Mataifa mawili kama suluhu ya mgogoro wa Israel na Palestina mwanzoni mwa wiki hii. Matamshi ya waziri mkuu huyo wa Israel ya kutotaka kuwepo kwa taifa la Palestina yanaonekana na wengi kama ndio yaliyomsaidia kushinda katika uchaguzi uliofanyika siku March 17 mwaka huu. Taarifa zinasema kuwa NETANYAHU amekiambia Kituo cha Televisheni cha Marekani, MSNBC, kwamba bado anabaki na...

Like
171
0
Friday, 20 March 2015
MARUBANI WA SHIRIKA LA NDEGE LA UJERUMANI LUFTHANSA WATANGAZA KUENDELEA NA MGOMO LEO
Global News

MARUBANI wa Shirika la ndege la Ujerumani Lufthansa wametangaza kwamba wataendelea na mgomo wao leo mgomo ambao tayari umewaathiri maelfu ya abiria na kushuhudia kufutwa kwa mamia ya safari kutokana na mzozo juu ya mpango wa malipo ya kustaafu. Msemaji wa Shirika la ndege la Lufthansa amesema nusu ya safari 1,400 za shirika hilo za ndani na zile za Ulaya kuingia na kuondoka Frankfurt na Munich zimefutwa hapo na kuathiri abiria 80,000. Mgomo huo wa siku moja awali ulikuwa umepangwa...

Like
361
0
Friday, 20 March 2015
MAREKANI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA IRAN
Global News

RAIS BARRACK OBAMA ametoa ujumbe katika kanda ya video kwa viongozi na raia wa Iran akisema kwamba hapajakuwa na wakati muafaka zaidi katika miongo kadha iliyopita kwa Marekani na Iran kutafuta uhusiano mpya. Katika ujumbe wa kusherehekea mwaka mpya wa Iran, OBAMA amesema Mataifa hayo mawili yana nafasi ya kihistoria ambayo haipaswi kupotea. Amesema mazungumzo kuhusu mpango wa nuklia wa Iran yamepiga hatua lakini ameonya kuwa kuna watu wanaopinga mazungumzo juu ya mpango huo kwa nchi zote mbili yaani Marekani...

Like
162
0
Friday, 20 March 2015
CHINA NA JAPAN KUFANYA MKUTANO WA KWANZA WA KIWANGO CHA JUU CHA USALAMA
Global News

CHINA na Japan wanafanya mkutano wa kwanza wa kiwango cha juu wa usalama katika muda wa miaka minne. Mkutano huo unaofanyika Tokyo unajumuisha maafisa kutoka wizara za mambo ya nje na ulinzi ambapo mazungumzo hayo yalisitishwa mnamo mwaka 2011 kutokana na hofu kuhusu visiwa vinavyozozaniwa Mashariki mwa bahari ya China. Pande zote zimesisistiza umuhimu wa mazungumzo ya kweli kudumisha amani....

Like
241
0
Thursday, 19 March 2015