Global News

BALOZI WA MAREKANI KOREA KUSINI ASHAMBULIWA KWA KISU
Global News

BALOZI wa Marekani nchini Korea Kusini ameshambuliwa kwa kisu usoni na pia katika kifundo cha mkono wake na mshambuliaji aliyekuwa akipiga kelele kuhusiana na suala la kugawanywa kwa kipande cha ardhi ya jumuiya yao. Mara tu baada ya shambulio hilo Rais wa Marekani Barack Obama amemtakia uponaji wa haraka msaidizi wake wa zamani Mark Lippert akimuombea uponaji wa haraka baada tu ya shambulio lililofanywa wakati wa hotuba ya asubuhi. Balozi huyo mwenye umri wa miaka 42 alikimbizwa hospitalini ambako alifanyiwa...

Like
179
0
Thursday, 05 March 2015
AHUKUMIWA MIAKA 75 JELA KWA KULAWITI MWANAE NA KUMPA HIV
Global News

Mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 44 amehukumiwa kutumikia kifungo cha miaka 75 jela nchini Kenya Hukumu hiyo imetolewa na mahakama ya watoto ya Nakuru baada ya kukutwa na hatia ya kushiriki mapenzi na mototo wake mwenye umri wa miaka 12 na kumuambukiza virusi vya...

Like
259
0
Thursday, 05 March 2015
FERGUSON: MEYA ATANGAZA KUWACHUKULIA HATUA POLISI DHIDI YA VITENDO VYA UBAGUZI WA RANGI
Global News

MEYA wa mji wa Ferguson, jimboni Missouri, ametangaza hatua zitakazochukuliwa kufuatia ripoti iliyoonyesha ushahidi dhidi ya polisi wa mjini humo kujihusisha na vitendo vya ubaguzi wa rangi. Meya JAMES KNOWLES amesema mwajiriwa mmoja toka Idara ya Polisi amefukuzwa kazi na wengine wawili wamelazimishwa kwenda likizo baada ya kushutumiwa kutuma barua pepe yenye ujumbe wa kibaguzi. KNOWLES amewaambia Waandishi wa Habari kuwa Idara itaongeza namba ya Maafisa wasio wazungu na kujikita...

Like
152
0
Thursday, 05 March 2015
MVUTANO WA DIGITALI WAMALIZIKA KENYA
Global News

MVUTANO kati ya Serikali ya Kenya na vyombo vya habari kuhusu kuhamia mfumo wa Digitali kutoka Analogia ambao umesababisha Vituo vinne vikubwa vya Televisheni nchini humo kutorusha matangazo hivi sasa umeisha. Vituo hivyo mfumo wake wa Analogia ulizimwa,vitaanza kurusha matangazo yake tena. Makubaliano hayo yamefikiwa March 03 mwaka huu kati ya Serikali na Vituo hivyo vikubwa vya Televisheni nchini Kenya NTV, QTV, KTN na Citizen TV ambavyo vimekubaliwa kurusha matangazo yao jijini Nairobi chini ya Mtandao wa Africa Digital Networks...

Like
147
0
Thursday, 05 March 2015
RAIA WA AUSTRALIA WAKABILIWA NA ADHABU YA KIFO BAADA YA KUKUTWA NA HATIA YA KUSAFIRISHA DAWA ZA KULEVYA
Global News

WATU  wawili  raia  wa  Australia  waliopatikana  na  hatia  ya kusafirisha  dawa  za  kulevywa   wamehamishwa   kutoka  jela mjini  Bali  nchini  Indonesia  leo  na  kupelekwa  katika  kisiwa kimoja  nchini  humo  ambako  watauwawa  kwa  kupigwa  risasi. Kwa  mujibu  wa  ripoti  za  vyombo  vya  habari  nchini  Australia, hatua  hiyo  ya  adhabu  ya  kifo  kwa  Myuran Sukumaran  na Andrew Chan imeongeza  wasiwasi  wa  kidiplomasia,  huku  kukiwa na  maombi  ya  msamaha  kwa  watu ...

Like
196
0
Wednesday, 04 March 2015
OBAMA APUUZIA ONYO LA NETANYAHU
Global News

RAIS Barack  Obama wa Marekani, ametupilia mbali onyo alilotoa waziri mkuu wa Israel kuhusu mpango wa Iran wa Nuclear katika hotuba yake tata kwa bunge la Marekani. Rais  Obama amesema Benjamin Netanyahu alishindwa kutoa suluhisho mbadala kuhusu suala kuu la jinsi ya kuizuia Teheran kutengeza silaha za Nuclear. Waziri Mkuu Netanyahu ambaye alialikwa kuhutubia bunge na viongozi wa chama cha Republican alishutumu mkataba uliowekwa kati ya mataifa ya magharibi na Iran na kudai kuwa ni hatari .  ...

Like
204
0
Wednesday, 04 March 2015
UMOJA WA NCHI ZA MAGHARIBI WATAKA HATUA KALI ZICHUKULIWE MZOZO WA UKRAINE
Global News

VIONGOZI wa nchi za Magharibi wamekubaliana kwamba hatua kali kutoka kwa Jumuiya ya Kimataifa zitahitajika iwapo kutatokea ukiukaji wa utekelezaji wa Mkataba wa kusitisha mapigano nchini Ukraine. Mkataba huo umesainiwa Mjini Minsk nchini Belarus Febrauari 12 mwaka huu kati ya majeshi ya Serikali ya Ukraine na Waasi wanaoiunga mkono Urusi. Rais wa Marekani BARACK OBAMA, mwenzake wa Ufaransa FRANCOIS HOLLANDE, Kansela wa Ujerumani ANGELA MERKEL, Waziri Mkuu wa Uingereza DAVID CAMERON na Waziri Mkuu wa Italia MATTEO RENZI wameshiriki katika...

Like
165
0
Wednesday, 04 March 2015
NETANYAHU AKOSOA JUHUDI ZA BARACK OBAMA
Global News

WAZIRI Mkuu wa Israel BENJAMIN NETANYAHU amelionya Bunge la Marekani kwamba mkataba na Iran uliopendekezwa hautazuia wala kupunguza uwezo wake wa kutengeneza mabomu ya nyuklia. Akilihutubia bunge hilo Bwana  NETANYAHU amezikosoa juhudi za Rais wa Marekani BARACK OBAMA kutafuta makubaliano na Iran kuhusu mpango wake wa nyuklia wenye utata. Bwana NETANYAHU ameonya kwamba utawala wa Bwana OBAMA unaifungulia mlango Iran kuelekea kutengeneza bomu la nyuklia.  ...

Like
208
0
Wednesday, 04 March 2015
ANGELA MERKEL AUNGA MKONO MPANGO MPYA WA UWEKEZAJI BARA LA ULAYA
Global News

KANSELA  wa  Ujerumani  ANGELA  MERKEL  ameeleza  kuunga  kwake  mkono mpango  mpya  wa  uwekezaji  katika  Bara  la  Ulaya. Mpango  huo  wa Uwekezaji  umependekezwa  mwaka  jana  na  Rais  wa  Halmashauri  ya Umoja  wa  Ulaya  JEAN-CLAUDE JUNCKER  ambapo ni   mpango  wa  Euro Bilioni 300 wa  kuifanya  bora  miundo Mbinu  katika  mataifa  ya  Ulaya. MERKEL  ameeleza  uungaji  wake  mkono  katika  mpango  huo , lakini amesema  mageuzi  zaidi  na  makubaliano  ya  Biashara  huru  na...

Like
182
0
Tuesday, 03 March 2015
UKRAINE: WAZIRI WA MAMBO YA KIGENI AONYESHA HOFU JUU YA MATARAJIO YA KUSITISHA MAPIGANO
Global News

WAZIRI  wa  Mambo  ya  Kigeni  wa  Ukraine  PAVLO KLIMKIN ameonesha  wasiwasi  wake    kuhusiana  na  matarajio kwamba  makubaliano  yanayoungwa  mkono  na  Umoja  wa Mataifa  ya  kusitisha  mapigano  na  waasi  wanaoiunga  mkono Urusi  yataendelea, wakati  akitoa  wito  wa  kuongezeka  kwa  kikosi cha  Kimataifa  cha kuangalia  makubaliano  hayo. Bwana KLIMKIN  amewaambia  Waandishi  Habari  mjini  Tokyo  kwamba  hali katika  eneo  la  mapigano ni  mbaya  na  ya  wasi wasi  licha  ya...

Like
192
0
Tuesday, 03 March 2015
MAJESHI YA IRAQ YAANZA OPERESHENI KUUKOMBOA MJI WA TIKRIT
Global News

IRAQ imeanzisha operesheni kubwa ya kuukomboa mji wa Tikrit unaodhibitiwa na kundi la Dola la Kiislamu. Wanajeshi Elfu-30 wa Iraq na wapiganaji wakisadiwa na ndege za kivita wamezishambulia ngome za wapiganaji wa jihadi wa kundi hilo ndani ya mji huo na maeneo yanaozunguka, katika harakati inayoelezwa kuwa kubwa kabisa kuwahi kufanywa kuyakomboa maeneo yanayodhibitiwa na Dola la Kiislamu. Vikosi vya Serikali ya Iraq vimekuwa vikisonga mbele kuelekea maeneo ya Kaskazini huku vikipata ushindi dhidi ya kundi hilo lakini mji wa...

Like
206
0
Tuesday, 03 March 2015