UKRAINE: WAZIRI WA MAMBO YA KIGENI AONYESHA HOFU JUU YA MATARAJIO YA KUSITISHA MAPIGANO

UKRAINE: WAZIRI WA MAMBO YA KIGENI AONYESHA HOFU JUU YA MATARAJIO YA KUSITISHA MAPIGANO

Like
196
0
Tuesday, 03 March 2015
Global News

WAZIRI  wa  Mambo  ya  Kigeni  wa  Ukraine  PAVLO KLIMKIN ameonesha  wasiwasi  wake    kuhusiana  na  matarajio kwamba  makubaliano  yanayoungwa  mkono  na  Umoja  wa Mataifa  ya  kusitisha  mapigano  na  waasi  wanaoiunga  mkono Urusi  yataendelea, wakati  akitoa  wito  wa  kuongezeka  kwa  kikosi cha  Kimataifa  cha kuangalia  makubaliano  hayo.

Bwana KLIMKIN  amewaambia  Waandishi  Habari  mjini  Tokyo  kwamba  hali katika  eneo  la  mapigano ni  mbaya  na  ya  wasi wasi  licha  ya makubaliano  hayo.

Amesema  bado  kuna  makombora  kadhaa yanavurumishwa  na  magaidi  mashariki  mwa  Ukraine.

Comments are closed.