CPJ yapatwa na hofu ya wafanyakazi wake kukamatwa

CPJ yapatwa na hofu ya wafanyakazi wake kukamatwa

Like
557
0
Thursday, 08 November 2018
Local News

Kamati ya Kimataifa ya Kuwalinda Waandishi wa Habari CPJ imezitaka Mamlaka nchini Tanzania kuwaachia huru wawakilishi wake wawili barani Afrika, Mratibu wa progam barani Afrika Angela Quintal na Muthoki Mumo mwakilishi wa CPJ kusini mwa jangwa la Sahara ambao wanadaiwa kukamatwa na Idara ya Uhamiaji nchini.

Muthoki Mumo

Angela Quintal

Kwa mujibu wa Taaarifa iliyotolewa na kuchapishwa kwenye tovuti ya CPJ, Afisa mmoja aliyejitambulisha kuwa ni mfanyakazi wa Idara ya Uhamiaji aliwakamata wafanyakazi hao wawili wa CPJ Angela Quintal na Muthoki Mumo, katika hotel waliyofikia jijini Dar es Salaam ambapo walikagua vitu walivyokuwa navyo na baadae kuchukua pasi zao za kusafiria.

Taarifa hiyo inadai Wafanyakazi hao ambao wamekuja nchini kwa masuala ya kikazi, inaelezwa kuwa waliondolewa hotelini na kupelekwa sehemu wasioijua.

Mkurugenzi mtendaji wa CPJ Joel Simon amesema wana wasiwasi na usalama wa wafanyakazi wao huku wakidai kuwa waliingia Tanzania ki uhalali.

Ametoa wito kwa mamlaka nchini kuwaachia na kuwarejeshea pia pasi zao hizo za kusafiria.

“Ni jambo la kutia wasi wasi mkubwa kuwa huenda simu ya Angela Quintal imetumiwa bila idhini yake. Hatujawasiliana na Angela Quintal au Muthoki Mumo tangua wakamatwe na tunaamini kuwa wote wanazuiliwa na mamlaka za Tanzani,” Joel Simon aliandika kwenye Twitter.

Hata hivyo akizungumza kwa njia ya simu Afisa Habari wa Idara ya Uhamiaji nchini Tanzania Ali Mtanda amesema hana habari kuhusiana na taarifa hiyo na kwamba bado hazijafika makao makuu na kutaka kupewa muda, ili kuweza kuthibitisha.

Hata hivyo taarifa ambazo bado hazijathibitisha zilizotufikia muda huu ni kwamba wafanyakazi hao wa CPJ hao wameachiliwa huru.

cc; BBCswahili

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *