CRISTIANO RONALDO AMWAGANA NA SHAYK

CRISTIANO RONALDO AMWAGANA NA SHAYK

Like
215
0
Wednesday, 21 January 2015
Slider

Mchezaji bora wa dunia Cristiano Ronaldo na mwanamitindo wa Urusi Irina Shayk wameripotiwa kuachana baada ya miaka mitano ya mahusiano yao.

Tetesi hizo zilianza kusambaa mara baada ya Shyk kukosa kuhudhuria kwenye sherehe za kutoa tuzo za mchezaji bora duniani wiki iliyopita na utata ulikuja zaidi pale muwakilishi wa mwanamitindo Shayk kuzungumza na waandishi wa habari huko marekani na kuweka wazi kuwa wawili hao hawapo pamoja tena

Mwanamitindo huyo mwenye umri wa miaka 29 alijizolea umaarufu zaidi duniani baada ya kucheza kwenye filamu yake ya kwanza ya ‘Hercules’ huko Hollywood mwaka jana.

Comments are closed.