DJOKOVIC AVUNJA REKODI YA IVAN LENDL

DJOKOVIC AVUNJA REKODI YA IVAN LENDL

Like
308
0
Monday, 17 November 2014
Slider

Bingwa namba moja katika mchezo wa Tennis, Novak atawazwa kuwa mshindi wa michuano ya ATP World Tour Finals huko jijini London baada ya Roger Federer kushindwa kucheza mchezo wa fainali kutokana na maumivu ya mgongo.

Federer aliyeshinda kwa seti 4-6 7-5 7-6(8-6) ndani masaa mawili na dakika arobaini na nane siku ya jumamosi dhidi ya Wawrinka ameomba radhi kutokana na kitendo hicho.

Huu ni ubingwa wan ne kwa MSerbia Djokovic ikiwa ni mara yake ya tatu mfululizo kutwaa taji hilo akifikia rekodi iliyowekwa na Ivan Lendl miaka ya themanini.

Toka mwaka 2014 katika michuano mbalimbali, Novak Djokovic amecheza michezo 66 akifungwa minne na kushinda sitini na mbili na kumfanya amalize akiwa bingwa namba moja duniani.

Comments are closed.