VAN GHAL KUMKOSA KIUNGO BLIND MECHI ZIJAZO

VAN GHAL KUMKOSA KIUNGO BLIND MECHI ZIJAZO

Like
237
0
Monday, 17 November 2014
Slider

Kiungo wa timu ya taifa ya Uholanzi na klabu ya Manchester United, Daley Blind anaweza kukaa nje ya uwanja kwa muda wa wiki sita baada ya kupata jeraha la goti katika mchezo wa kuwania kuingia michuano ya Ulaya mwaka 2016 huko nchini Ufaransa.

Katika mchezo huo ambao timu ya Taifa ya Uholanzi iliibuka na ushindi mnono wa magoli 6-0 dhidi ya Latvia, Blind aliumia mnamo dakika ya 20 ya mchezo kwa kugongana na mchezaji Eduards Visnakovs.

Kuumia kwa kiungo huyo ni pigo kubwa kwa klabu ya Manchester United chini ya aliyekuwa kocha wa Uholanzi, Louis Van Ghal akiwa mpaka sasa ameshawapoteza wachezaji muhimu katika kikosi cha kwanza akiwemo David De Gea, Phil Jones, Michael Carrick, radamel Falcao huku Cris Smalling akiwa na adhabu.

Manchester United inayoshika nafasi ya 7 katika msimamo wa ligi kuu nchini England siku ya jumamosi itasafiri kwenda jijini London kumenyana na klabu ya Arsenal inayoshika nafasi ya 6.

Comments are closed.