EBOLA: RAIS OBAMA ALIOMBA BUNGE DOLA BILIONI 6.2 KWA AJILI YA MFUKO WA DHARURA

EBOLA: RAIS OBAMA ALIOMBA BUNGE DOLA BILIONI 6.2 KWA AJILI YA MFUKO WA DHARURA

Like
210
0
Thursday, 06 November 2014
Global News

RAIS BARACK OBAMA wa Marekani ameliomba Bunge la nchi hiyo Dola Bilioni 6 nukta 2 kwa ajili ya Mfuko wa Dharura wa kupambana na maradhi ya Ebola katika eneo la Magharibi mwa Afrika, na kuzuia uwezekano wa Ugonjwa huo kusambaa hadi Marekani.

Sehemu ya mfuko huo Dola Bilioni Mbili zinatarajiwa kukabidhiwa kwa Shirika la Marekani la Msaada wa Kimataifa – USAID, huku Dola Bilioni 2 nukta 4 zikienda Idara ya Afya na Huduma za Binadamu nchini humo.

Taarifa zaidi zimebainisha kuwa pesa zilizobakia Dola Bilioni 1 nukta 5 zitatumika katika dharura kama vile kushughulikia kukithiri kwa Maambukizi Magharibi mwa  Afrika na kuwapa Chanjo wahudumu wa Afya nchini Marekani.

OBA

Comments are closed.