ERIC ABIDAL ATANGAZA KUSTAAFU SOKA

ERIC ABIDAL ATANGAZA KUSTAAFU SOKA

Like
219
0
Friday, 19 December 2014
Slider

Beki wa Kimataifa wa Ufaransa na klabu ya Olympiacos, Eric Abidal ametangaza kustaafu kucheza soka ikiwa ni takribani miaka kumi na nne toka aanze kucheza soka la kulipwa.

Abidal alijiunga na klabu ya Olympiacos msimu huu na kusaini mkataba wa miaka miwili uliokuwa uishe msimu wa 205/2016 lakini ameamua kuuvunja kwasababu za kiafya.

Beki huyo wa kushoto amekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kansa toka mwaka 2011 na kumfanya akose michezo mingi akiwa na klabu ya FC Barcelona walioamua kumpa heshima ya kubeba taji la klabu bingwa Ulaya baada ya kuifunga klabu ya Manchester United kwa magoli 3-1.

Abidal sasa atajiunga na klabu ya FC Barcelona kama mkufunzi wa vijana wa La Masia, moja kati ya vituo vya soka vinavyosifika kwa kutoa vipaji mbalimbali kama Messi, Iniesta, Xavi, Fabregas na Puyol.

Fuatilia kipindi cha E sport kila siku kuanzia saa moja jioni kwa habari zaidi

Comments are closed.