FA YAMUADHIBU BALLOTELI KUFUATIA VITENDO VYA UBAGUZI WA RANGI

FA YAMUADHIBU BALLOTELI KUFUATIA VITENDO VYA UBAGUZI WA RANGI

Like
251
0
Friday, 19 December 2014
Slider

Chama cha soka cha nchini England (FA) kimemuadhibu mshambuliaji wa klabu ya Liverpool, Mario Balloteli kwa kumfungia kutocheza mchezo mmoja wa ligi kuu nchini England na kumtaka alipe fidia ya kiasi cha paundi ishirini na tano elfu baada ya mchezaji huyo kukutwa na hatia ya vitendo vya ubaguzi.

Hatua hiyo imefikiwa na chama hicho baada ya Muitaliano huyo kutuma ujumbe ulionyesha vitendo vya kibaguzi katika mtandao wa kijamii wa twitter kwa kuandika “ruka juu kama mtu mweusi ila tafuta fedha kama jew (watu wenye asili ya Israel).” Balotelli

Pamoja na adhabu hiyo mshambuliaji huyo wa timu ya taifa ya Italia ametakiwa kuweza kuhudhuria mafunzo maalum uya elimu dhidi ya vita ya kupinga ubaguzi wa rangi katika kituo atakachopangiwa.

Balotelli aliyejiunga na majogoo hao wa jiji akitokea klabu ya AC Milan kwa daua la paundi million 16 atakosa mchezo wa jumapili dhidi ya Arsenal huku klabu ya Liverpool ikiwa inashika nafasi ya kumi na moja katika msimamo wa ligi kuu nchini England.

Comments are closed.