GIANFRANCO ZOLA ATEULIWA KUWA KOCHA MPYA WA CAGLIARI

GIANFRANCO ZOLA ATEULIWA KUWA KOCHA MPYA WA CAGLIARI

Like
332
0
Thursday, 25 December 2014
Slider

Mchezaji wa zamani wa klabu ya Chelsea na timu ya taifa ya Italy, Gianfranco Zola ameteuliwa kuwa kocha mpya wa klabu ya Cagliari kwa kuchukua nafasi ya Zdenek Zeman.

Uongozi wa Cagliari umefikia maamuzi hayo baada ya kuona matokeo mabovu chini ya kocha Zeman aliyewaacha katika nafasi ya 17 ndani ya ligi kuu nchini Italy (Serie A).

Zola aliyewahi kuvinoa vikosi mbalimbali kama West Ham na watford anataraji kuanza kukinoa kikosi cha Cagliari mnamo siku ya jumapili ya tarehe 28 mwezi wa 12, 2014 huku mechi yake ya kwanza itakuwa tarehe 6 mwezi januari dhidi ya Palermo.

Legendari huyo wa klabu ya Chelsea alimalizia maisha yake ya soka ndani ya Cagliari na sasa anakazi ya kuweza kuikomboa klabu hiyo iliyopata ushindi katika michezo miwili tu ndani ya michezo kumi na sita ya mwanzo isishuke daraja.

Comments are closed.