GIANNI KUWANIA URAIS FIFA

GIANNI KUWANIA URAIS FIFA

Like
167
0
Tuesday, 27 October 2015
Slider

katibu Mkuu wa shirikisho la mpira wa miguu barani Ulaya Gianni Infantino ameingia kwenye kinyang’anyiro cha kuwania Urais wa shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA.

Infantino alijumuika kwenye orodha ya wanaowania nafasi hiyo saa chache kabla ya siku ya mwisho ya kupokea maombi ambayo ni jumatatu

Maamuzi haya ya Infantino kuungana Michel Platini kwenye maombi hayo ili kuweza kuchukua nafasi ya Sepp Blatter, 79. Kunazidi kuongeza kasi ya matarajio ya kuwa na mchuano mkali.

Rais wa shirikisho la mpira wa miguu barani Asia Sheikh Salman bin Ebrahim Al Khalifa pia nae amethibitisha ushiriki wake kwenye zoezi hilo

Fifa bado haijatoa orodha ya majina yaliyopitishwa kwenye mchuano huo.

 

Comments are closed.