Hali ya Kingwalla Yazidi Kuimarika

Hali ya Kingwalla Yazidi Kuimarika

Like
654
0
Tuesday, 14 August 2018
Local News
HALI ya Waziri wa Maliasili na Utali, Dkt. Hamisi Andrea Kigwangalla imeendelea kuimarika vizuri kutokana na matibabu anayopatiwa katika Hospitali ya Taifa, Muhimbili alikolazwa baada ya kupata ajali ya gari akiwa mkoani Arusha kuelekea Dodoma kikazi.
Picha zinaonesha Kigwangalla akiwa amepata nafuu na kutoka nje ya Jengo la Hospitali hiyo jambo linaloonyesha faraja huenda akapona hivi karibuni.
Mbunge huyo wa Nzega (CCM) alipata ajali wiki chache zilizopita baada ya gari lake kupinduka na kusababisha kifo cha Afisa habari wake, Hamza Temba aliyezikwa mkoani Tanga.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *