HATMA YA MAKUNDI KUFAHAMIKA COPA AMERIKA

HATMA YA MAKUNDI KUFAHAMIKA COPA AMERIKA

Like
298
0
Monday, 24 November 2014
Slider

Mataifa mbalimbali kutoka barani Amerika ya Kusini yatajua hatma yao katika upangwaji wa makundi ya michuano ya Copa Amerika inayotarajiwa kufanyika mwaka 2015 huko nchini Chile.

Katika jiji la Vina Del Mar mataifa kumi na mbili yatagawanywa katika makundi matatu yatakayojumuisha timu nne kila kundi kwenye hatua ya kwanza.

Chile ambaye ndio mwenyeji wa michuano hiyo amewekwa katika kapu namba moja pamoja na timu ya Brazil na Argentina huku Uruguay ambaye ni bingwa mtetezi wa michuano hiyo amewekwa katika kapu namba mbili linalojumuisha na timu za Colombia na Mexico (kaalikwa).

Mataifa mengine yanasubiri upangwaji huo wa makundi ni Ecuador, Peru, Paraguay, Venezuela, Bolivia na Jamaica ambaye ni mualikwa katika michuano hiyo iliyoanzishwa miaka tisini na nane iliyopita.

Comments are closed.