FORMULA 1 – LANGALANGA LEWIS AHAIDI MAKUBWA BAADA YA USHINDI

FORMULA 1 – LANGALANGA LEWIS AHAIDI MAKUBWA BAADA YA USHINDI

Like
234
0
Monday, 24 November 2014
Slider

 

Dereva wa magari ya Mercedes, Lewis Hamilton ameahidi kufanya makubwa zaidi katika mashindano mashindano ya Formula 1 baaada ya kufanikiwa kubeba taji la mwaka huu.

Hamilton amefanikiwa kubeba taji kwa tofauti ya alama sitini na saba dhidi ya mpinzani wake wa karibu, Nico Rosberg likiwa ni taji lake la pili baada ya lile la kwanza kulitwaa mwaka 2008 akiwa na timu ya McLaren.

Akiwa ni mmoja kati ya madereva saba kuwahi kutwaa taji hilo mara mbili katika historia ya Formula 1 na wanne kutoka visiwa vya Uingereza amepanga kuvunja rekodi ya Michael Schumacher ya kutwaa mataji saba.

Hamilton amesema anajua fika kuwa kabla ya kufikia rekodi ya Schumacher anatakiwa kufikia rekodi ya Juan Manuel Fangio aliyetwaa taji hilo mara tano huku Sebastian Vettel ambaye amehamia timu ya Ferrari akiwa na mataji manne kibindoni.

Comments are closed.