HATMA YA PISTORIUS KUFAHAMIKA LEO

HATMA YA PISTORIUS KUFAHAMIKA LEO

Like
154
0
Tuesday, 03 November 2015
Slider

MAHAKAMA kuu ya rufaa nchini Afrika Kusini huenda ikaamua leo hii iwapo Mwanariadha mlemavu wa miguu Oscar Pistorius amemuua kwa kukusudia au bila kukusudia mpenzi wake wakati wa sikukuu ya wapendanao mwaka 2013.

Mwanariadha huyo, hivi karibuni alianza kutumikia kifungo cha nyumbani akiwa tayari amekwisha kutumikia kifungo cha mwaka mmoja kati ya miaka mitano aliyohukumiwa jela.

Endapo majaji wa mahakama hiyo kuu ya rufaa watageuza maamuzi ya awali na kuwa kesi ya mauaji, Oscar Pistorius atarejeshwa tena jela na kutumikia kifungo cha miaka kumi na mitano.

Comments are closed.