UTATA CHANZO CHA AJALI YA NDEGE MISRI

UTATA CHANZO CHA AJALI YA NDEGE MISRI

Like
174
0
Tuesday, 03 November 2015
Global News

UTATA umeendelea kujitokeza katika ajali ya ndege iliyoanguka katika rasi ya Sinai huko nchini Misri na kuua abiria 224 waliokuwemo kwenye ndege hiyo.

Wakati mkuu wa Mamlaka ya Anga ya nchini Urusi Aleksandar Neradko akisema kuwa ni mapema kutabiri chanzo cha ajali hiyo, lakini wamiliki wa ndege hiyo wamesema ajali imesababishwa na nguvu ya mvutano kutoka kutoka nje.

 

Kwa upande wake Balozi wa Urusi nchini Misri Serge Kirpichenko amesema itachukua muda mrefu kabla ya kupata taarifa sahihi kutoka kwenye kisanduku cheusi kilichorekodi tukio hilo.

Comments are closed.