HOFU YA EBOLA YATANDA MAREKANI

HOFU YA EBOLA YATANDA MAREKANI

Like
248
0
Wednesday, 01 October 2014
Global News

Hali hiyo imekuja mara baada ya Mgonjwa wa kwanza wa ugonjwa hatari wa virusi vya Ebola kugundulika nchini Marekani, na kuthibitishwa katika mji wa Dallas, Texas.

Maafisa katika kituo cha afya cha Texas katika hospitali ya Presbyterian wamesema mgonjwa ambaye hakutajwa ametengwa katika hospitali hiyo.

ebola_suit

watoa huduma wa afya

Jumatatu, maafisa wa kituo cha afya cha Texas katika hospitali ya Presbyterian ya Dallas wamesema mgonjwa ambaye hakutajwa jina alikuwa akichunguzwa virusi vya Ebola na ametengwa katika hospitali hiyo.

Shirika la Afya Duniani, WHO limesema mpaka sasa zaidi ya watu 3,000 wamekufa kutokana na virusi vya Ebola, wengi wa waliokufa ni kutoka Liberia.

Nchini Nigeria, nchi yenye idadi kubwa ya watu barani Afrika kuna wagonjwa 19 waliothibitika kuugua ugonjwa wa Ebola na watu wanane wamekufa tangu mgonjwa wa kwanza kuthibitishwa nchini humo mwezi Julai..

Kuna mgonjwa mmoja aliyethibitika nchini Senegal, lakini hakuna taarifa za kifo mpaka sasa.

Ebola ni ugonjwa hatari wa virusi kuwahi kuzuka duniani.

Comments are closed.