JOHN KERRY: URUSI BADO HAIJATIMIZA MASHARTI KUSITISHA MAPIGANO

JOHN KERRY: URUSI BADO HAIJATIMIZA MASHARTI KUSITISHA MAPIGANO

Like
248
0
Thursday, 26 February 2015
Global News

WAZIRI wa  mambo  ya  kigeni  wa  Marekani John Kerry  amesema  Urusi bado  haijatimiza masharti  ya  makubaliano ya Minsk kuhusu usitishaji wa mapigano.

Kerry  amewaambia  wabunge  mjini  Washington kwamba Urusi na  wapiganaji  wanaoiunga  mkono  Urusi hawaheshimu masharti ya  makubaliano.

Wakati  huo  huo , rais  wa  Urusi Vladimir Putin ameonya  kwamba Urusi inaweza  kusitisha upelekaji  wa  gesi  nchini Ukraine. Kansela  wa Ujerumani  Angela  Merkel ameionya  Urusi  kwamba  vikwazo  vinaweza kutekelezwa.

 

Comments are closed.