EBOLA: WHO YATANGAZA KUPUNGUA KWA MAAMBUKIZI MAPYA AFRIKA MAGHARIBI

EBOLA: WHO YATANGAZA KUPUNGUA KWA MAAMBUKIZI MAPYA AFRIKA MAGHARIBI

Like
194
0
Thursday, 26 February 2015
Global News

SHIRIKA la  afya  ulimwenguni  WHO limetangaza kwamba  maambukizi mapya  ya  ugonjwa  wa  Ebola katika  mataifa  ya  Afrika  magharibi yamepungua.

Wiki  iliyopita, kulikuwa  na  zaidi ya  watu 100 walioambukizwa  ugonjwa  huo nchini  Sierra Leone, Guinea  na  Liberia.

Wiki  hii , maambukizi  mapya  ya  Ebola  yamepungua  chini  ya  watu 100, kwa  mujibu  wa  shirika  hilo  la  afya  ulimwenguni.

Hata  hivyo kituo  cha  taifa  kinachohusika  na  suala  la  ugonjwa  wa Ebola  nchini  Sierra Leone  kimesema  wagonjwa  wameongezeka.

 

Comments are closed.