TGNP YAITAKA JAMII KUISHI KWA KUFANYA TAFITI

TGNP YAITAKA JAMII KUISHI KWA KUFANYA TAFITI

Like
220
0
Thursday, 26 February 2015
Local News

MTANDAO wa Kijinsia Tanzania-TGNP umeitaka jamii kuishi kwa kufuata mbinu za kiraghibishi yaani utafiti ili kumuwezesha mtu kutambua nafasi yake na uwezo wa kubadilisha mazingira ili kuleta maendeleo nchini.

Akizungumza katika semina ya Uraghibishi,mtafiti Mkuu kutoka TGNP AGNESS LUKANGA amesema kuwa endapo jamii itaweza kuishi kwa kufuata njia za Uraghibishi itaweza kujitegemea ikiwa ni pamojua na kuhamasisha mtu kufanya kitu ambacho kitaleta maendeleo katika jamii.

Ameeleza kumekuwa na tabia ya baadhi ya watu kutoa maamuzi ya mambo mbalimbali katika jamii hali inayopelekea kushindwa kutambua matatizo yanayowakabili hasa katika jamii.

 

 

Comments are closed.