John Terry: Kapteni wa zamani wa England na Chelsea astaafu soka

John Terry: Kapteni wa zamani wa England na Chelsea astaafu soka

Like
818
0
Monday, 08 October 2018
Sports

Aliyekuwa kapteni wa timu ya taifa ya England na Chelsea John Terry amestaafu katika soka.

Terry, mwenye umri wa miaka 37, hajaichezea klabu yoyote tangu aondoke timu ya mabingwa Aston Villa msimu wa joto.

Mlinzi huyo alitoa tangazo hilo kwenye akaunti yake ya Instagram, akisema: “Baada ya miaka 23 kama mchezaji wa soka, nimeamua sasa ndio muda muafaka kwangu mimi kustaafu kutoka mchezo wa soka.”

Terry, aliyejinyakulia mataji 78 England, aliondoka Chelsea mnamo 2017 baadaya kuichezea klabu hiyo ya London kwa miongo miwili.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *