KAMANDA MKUU WA LRA ALIEJISALIMISHA AKABIDHIWA KWA WANAJESHI WA UGANDA

KAMANDA MKUU WA LRA ALIEJISALIMISHA AKABIDHIWA KWA WANAJESHI WA UGANDA

Like
216
0
Wednesday, 14 January 2015
Global News

 KAMANDA MKUU wa kundi la waasi la LRA nchini Uganda, aliyejisalimisha wiki jana, Dominic Ongwen , amekabidhiwa kwa wanajeshi wa Uganda walio katika Jamuhuri ya Afrika ya kati.

Muasi huyo, Dominic Ongwen, anasemekana kuwa Naibu kiongozi wa kundi hilo Joseph Kony na alikamatwa na wanajeshi wa Marekani wiki jana ingawa waasi wa Seleka wanasema wao ndio waliomkamata.

Waasi hao wanasema kwamba walimkatama Ongwen baada ya makabiliano ya muda ingawa jeshi la Marekani lilisitiza kuwa alijisalimisha na tangu hao wamekuwa wakimzuilia.

Comments are closed.