KIPINDUPINDU: KASI YA MAAMBUKIZI YAPANDA ARUSHA NA MWANZA

KIPINDUPINDU: KASI YA MAAMBUKIZI YAPANDA ARUSHA NA MWANZA

Like
230
0
Monday, 04 January 2016
Local News

 

IMEELEZWA kuwa licha ya kupungua kwa maambukizi mapya katika baadhi ya Mikoa, kasi ya kukuwa kwa maambukizi ya  ugonjwa wa Kipindupindu imeendelea kupanda katika Mikoa ya Mwanza na Arusha ambapo katika Mkoa wa Arusha maambukizi yamepanda  kutoka wagonjwa wapya 60 hadi wagonjwa wapya 111 kwa wiki na katika Mkoa wa MWanza maambukizi yamepanda kutoka  wagonjwa wapya 45 hadi 66 kwa wiki.

Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto, Dokta Ahmis Kigwangala wakati wa utoaji taarifa ya wiki kwa Waandishi wa habari kuhusu hali ya kipindupindu nchini.

Comments are closed.