KUPIGA KELELE NI UCHAFUZI WA MAZINGIRA

KUPIGA KELELE NI UCHAFUZI WA MAZINGIRA

5
628
0
Wednesday, 30 June 2021
Local News

Katika kukabiliana na uchafuzi wa mazingira unaosababishwa na kelele serikali imewaelekeza  wamiliki wa maeneo ya burudani na starehe kuzingatia matumizi ya vipima kelele na vizuia sauti kama inavyoelekezwa kwenye masharti ya leseni zao. Hili ni kwa sababu ya kulinda afya za wananchi kutokana na athari za kelele na mitetemo.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais,Muungano na Mazingira Seleman Jaffo wakati akiongea na vyombo vya habari Juni 29 kuhusu udhibiti wa uchafuzi wa Mazingira unaosababishwa na vitu hivyo.

“Kila mwananchi ahakikishe shughuli anazofanya haisababishi kero ya kelele na mitetemo, Wamiliki wa kumbi za starehe na burudani wahakikishe sauti zinazozalishwa katika shughuli zao hazizidi viwango vinavyokubalika kwa mujibu wa sheria. Hili tumeazimia wenye kumbi za starehe na burudani isiwe starehe ya kwako na watu wengine ikawa kero kwa watu wengine, Sauti zinazotoka zisidi viwango vilivyowekwa kwa mujibu wa sheria na kanuni”.- Amesema Jaffo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *