LIBERIA YAONDOA SHERIA YA EBOLA

LIBERIA YAONDOA SHERIA YA EBOLA

Like
339
0
Friday, 14 November 2014
Global News

RAIS wa Liberia ELLEN JOHNSON SIRLEAF ameondoa sheria ya hali ya hatari ambayo ilikuwa imetangazwa nchini humo katika juhudi za kudhibiti kuenea kwa maradhi ya Ebola, ambayo yaliizonga nchi hiyo na nyingine mbili jirani katika kanda ya Afrika Magharibi.

Katika hotuba yake kwa taifa Rais SIRLEAF amesema kuondolewa kwa sheria hiyo hakumaanishi kwamba mlipuko wa ugonjwa huo umemalizika.

Amebainisha kuwa Maendeleo ya kutosha yamepatikana katika vita dhidi ya maradhi hayo kuwezesha kuondolewa kwa sheria hiyo.

Comments are closed.