MAREKANI, INDIA MAMBO SHWARI

MAREKANI, INDIA MAMBO SHWARI

Like
255
0
Friday, 14 November 2014
Global News

MAREKANI na India zimesema zimepata muafaka juu ya mzozo uliohusu ruzuku ya chakula nchini India, ambayo mwaka jana ilikwamisha makubaliano ya kibiashara katika Shirika la Kimataifa la Biashara, WTO.

India imekataa kutia saini makubaliano hayo muhimu Julai mwaka jana, ikitaka kwanza kuhakikishiwa hazina kubwa ya chakula nchini humo.

Kulinagana na makubaliano yaliyofikiwa, hazina ya chakula ya India haitakabiliwa na changamoto zozote kutokana na kanuni za WTO, hadi pale suluhisho la kudumu kuhusu suala hilo litakapokuwa limepatikana.

Comments are closed.