Majambazi wachomoa mashine ya ATM ukutani

Majambazi wachomoa mashine ya ATM ukutani

Like
769
0
Tuesday, 02 April 2019
Global News

Majambazi wamenyofoa na kutokomea na mashine ya kielektroniki ya kutolea pesa nchini Ireland ya Kaskazini.

Majambazi hao walitumia tingatinga ambalo pia waliliiba katika kunyofoa ATM hiyo kutoka kwenye ukuta wa duka moja katika Kaunti ya Antrim.

Tukio hilo limetokea saa tisa ya usiku wa Jumatatu. Polisi wamethibitisha kuwa jengo hilo limeharibiwa vibaya.

Majambazi wamenyofoa na kutokomea na mashine ya kielektroniki ya kutolea pesa nchini Ireland ya Kaskazini.

Majambazi hao walitumia tingatinga ambalo pia waliliiba katika kunyofoa ATM hiyo kutoka kwenye ukuta wa duka moja katika Kaunti ya Antrim.

Tukio hilo limetokea saa tisa ya usiku wa Jumatatu. Polisi wamethibitisha kuwa jengo hilo limeharibiwa vibaya.

Majambazi wa ATM

“Tulipokea simu kuhusu tukio hilo mishale ya saa 9:25 usiku kuwa tingatinga linaungua moto nje ya duka ambalo ATM imechomolewa,” Inspekta wa Polisi Richard Thornton amesema.

“ATM imenyofolewa ukutani na kuharibu jengo ilipokuwa imewekwa…tunawataka mashuhuda wajitokeze, hususan walioiona gari ya rangi ya fedha.”

Mwezi uliopita, polisi walitangaza kuundwa kwa kikosi kipya cha kupambana na wizi wa mashine za ATM.

Toka ulipoanza mwaka 2019, mashine saba za ATM zimeibiwa. Polisi pia wanaamini kuna makundi kadhaa ya majambazi ambayo yanajihusisha na wizi wa mashine hizo.

Wamiliki wa maduka sasa wanaonesha uoga wao juu ya kuweka mashine hizo kwenye maeneo yao ya biashara na tayari watu kadhaa wametahadharisha endapo wizi huo utaendelea basi watalazimika kuzitoa mashine hizo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *