MALI YATANGAZA KIKOSI CHA AWALI KUELEKEA MICHUANO YA KOMBE LA MATAIFA AFRIKA 2015

MALI YATANGAZA KIKOSI CHA AWALI KUELEKEA MICHUANO YA KOMBE LA MATAIFA AFRIKA 2015

Like
319
0
Monday, 29 December 2014
Slider

Kocha msaidizi wa timu ya taifa ya Mali, Cheick Omar Kone ametangaza kikosi cha awali kinachotaraji kwenda kushiriki michuano ya kombe la mataifa ya Afrika mwezi januari mwaka 2015 huko nchini Equatorial-Guinea.

Kikosi hicho ambacho ni cha awali kabla ya kile cha mwisho kutangazwa mnamo tarehe tatu januari 2015 kimeshuhudia mshambuliaji wa klabu ya Metz, Modibo Maiga akirejea kundini baada ya kutoitwa kwa kipindi kirefu ndani ya timu hiyo.

Abdou Traore na Cheick Diabate wanaokipiga katika klabu ya Bordeaux nao nwamejumuishwa huku golikipa wa klabu ya Ajaccio Oumar Sissoko akiachwa.

Mali inayoongozwa na kocha raia wa Poland Henry Kasperczak inataraji kucheza mechi za kirafiki dhidi ya Afrika ya kusini na Tunisia kujiandaa na michuano hiyo itakayoanza tarehe 17 januari 2015.

Comments are closed.