MOUNRINHO: KUNA KAMPENI INAENDESHWA KUIANGUSHA CHELSEA LIGI KUU YA ENGLAND

MOUNRINHO: KUNA KAMPENI INAENDESHWA KUIANGUSHA CHELSEA LIGI KUU YA ENGLAND

Like
374
0
Monday, 29 December 2014
Slider

Kocha wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amesema kuna kampeni inaendeshwa dhidi ya klabu yake ili isifanye vizuri ndani ya ligi kuu nchini England kwa kuwashawishi marefarii kutotoa maamuzi sahihi.

Kocha huyo raia wan chini Ureno anayesifika kwa ubwatukaji amewashutumu makocha wenzake, watangazaji wa michezo pamoja na wachambuzi kuwa wanachangia kwa kiasi kikubwa klabu ya Chelsea kuandamwa na maamuzi ambayo siyo sahihi ndani ya uwanja.

Maneno hayo ameyatoa baada ya kushuhudia mchezaji Cesc Fabregas kunyimwa penalty katika mchezo wa jana dhidi ya Southampton na matokeo yake alilimwa kadi ya njano kwa kile refarii wa mchezo huo Taylor kutafsiri kuwa alijiangusha ndani ya eneo hilo la hatari.

Fabregas_3179732

Wachezaji wa Chelsea wamekuwa wakishutumiwa kujiangusha kutafuta penalty, kocha wa West Ham alimshutumu beki wa klabu hiyo Branoslav Ivanovic huku Cahill, Diego Costa nao pia walishutumiwa.

Comments are closed.