Marekani inapima hatua za kujibu shambulio ‘kemikali nchini Syria

Marekani inapima hatua za kujibu shambulio ‘kemikali nchini Syria

1
1106
0
Thursday, 12 April 2018
Global News

Marekani inasema kuwa “tayari ana maamuzi mengi” za kujibu shambulio linaloshukiwa kuwa la kikemikali nchini Syria, huku viongozi wa magharibi wakiendelea kupima hatua za kijeshi.
Msemaji wa Ikulu ya White House Sarah Sanders amewaambia wandishi wa habari kuwa hakuna ushahidi wa mwisho uliokwisha chukuliwa juu ya mashambulio ya kijeshi.
Lakini amesema Marekani inaziwajibisha Urusi na Syria kwa tukio hilo.

Baraza la Kitaifa la Usalama la Marekani litakutana Alhamisi, huku waziri mkuu wa Uingereza PM Theresa May akiitisha mkutano wa baraza la mawaziri kujadili tukio hilo la Syria.
Wanaharakati, wahudumu wa uokozi na madaktari wanasema makumi ya watu walikufa katika mji unaodhibitiwa na waasi wa Douma Jumamosi.

Comments are closed.