Zuckerberg akiri kosa lake na kuomba radhi

Zuckerberg akiri kosa lake na kuomba radhi

1
352
0
Thursday, 12 April 2018
Global News

Mkurugenzi Mtendaji wa Facebook Mark Zuckerberg ametoa maelezo katika Bunge la Marekani- Congress kwa mara ya kwanza Jumanne, akijibu wasiwasi ulioelezwa na wabunge juu ya kushindwa kwa mtandao wa jamii maarufu kulinda taarifa zao.
Taarifa hizo za siri za watumiaji wanaofikia milioni 87 ulimwenguni zilizotumiwa na kampuni yenye kujishughulisha na siasa- Cambridge Analytica iliyokuwa na mafungamano na Trump.

Mahojiano hayo yanaendelea Jumatano wakati Zuckerberg atakapokutana katika raundi ya pili kujibu maswali mbele ya jopo la Wabunge wa Marekani.

Mkurugenzi huyo Mark Zuckerberg amekiri kuwa :”Hilo lilikuwa kosa kubwa na ni kosa langu mimi mwenyewe na naomba radhi. Nilianzisha matandao wa Facebook, niliusimamia na nina wajibika kwa kitu chochote kinachotokea.”

Wachambuzi wanasema ni kosa ambalo liliruhusu kampuni ya kisiasa ya Cambridge Analytica kupata taarifa kwa kupitia programu iliyotengenezwa na kampuni nyingine, ambayo ili ingilia taarifa binafsi za mamilioni ya wanaotumia Facebook duniani.

Marc Rotenberg wa kituo cha kutunza taarifa za siri za kielektroniki amesema: “Ni suala nyeti kwa Facebook kwa njia nyingi. Kuhakikisha bei ya hisa zao zinanyanyuka, watu wana wasiwasi mkubwa juu ya mustakbali wa kampuni hiyo. Lakini nafikiri vipi Facebook itaweza kuendelea kufanya shughuli zake kama ilivyo kwani ni suala la wazi. Nafikiri mjini Washington na maeneo mengine, utashuhudia shinikizo la kuwepo mabadiliko ya kweli.

Mabadiliko yaliyoanza katika mahojiano yasiyo ya kawaida kabisa yakiendeshwa na nusu ya Baraza la Seneti ya Marekani.

Seneta Richard Durbin (Mdemokrati) alimuuliza Zuckerberg: “Je, uko radhi kutuambia jina la hoteli uliofikia jana usiku?” “Um, uh, hapana,” alijibu Zuckerberg.

Seneta Durbin : “Kama ulituma ujumbe kwa mtu yoyote wiki hii, unaweza kutujulisha majina ya watu hao uliowasiliana nao?’

“Seneta, hapana, pengine sitopendelea kufanya hivyo hadharani hapa,” alijibu mkurugenzi huyo wa Facebook.

“Nafikiri pengine hilo ndio suala zima. Haki yako ya kutoingiliwa maisha yako binafsi.”

Hata hivyo Zuckerberg ameahidi mabadiliko. Amesema iwapo tutagundua kuwa mtu yoyote alitumia taarifa za watu kinyume cha utaratibu, tuta wafungia kutumia Facebook na kumfahamisha kila aliyeathirika.”

Baadhi ya maseneta wamesema kuwa kuongeza uwazi katika mitandao ya jamii lazima iwe ni hatua ya pili baada ya hapa.

“Mmarekani wa hali ya kati hajui chochote pale mitandao inapowapeleka, umeona misamiati na masharti yaliyopo Facebook, mimi ni wakili, lakini sikuweza hata kufahamu maelezo ya ibara ya kwanza.”

Pamoja na kuwa baadhi ya maseneta wanatambua Facebook inahitaji kuwa na mfumo wa kibiashara unaoingiza kipato kwa kutumia taarifa za watu binafsi kwa ajili ya kuwavutia watangazaji.

“Hakuna kitu kilichokuwa bure katika maisha, kila kitu kinahusisha biashara, iwapo unafikiri unataka kitu bila ya kulipia.”

Mahojiano ya Zuckerberg na Bunge la Marekani limeibua mazungumzo.

“Je, utawafiki sheria ambayo itakutaka uwafahamishe watumiaji wa mitandao ya jamii kunapotokea uvunjifu wa sheria katika kipindi cha saa 72,” aliuliza Seneta Amy Klobuchar (Mdemokrati). Zuckerberg amejibu kuwa jambo hilo linafaa.

Comments are closed.