Meng Hongwei: China yathibitisha inamzuia mkuu wa Interpol aliyepotea

Meng Hongwei: China yathibitisha inamzuia mkuu wa Interpol aliyepotea

Like
511
0
Monday, 08 October 2018
Global News

China imethibitisha inamzuia mkuu wa Interpol aliyepotea Meng Hongwei.

Beijing imesema alikuwa anachunguzwa na tume ya kupambana na rushwa nchini humo kwa ukiukaji wa sheria.

Meng, ambaye pia ni naibu waziri wa wizara ya usalama wa umma China, aliarifiwa kupoeta baada ya kusafiri kutoka mji wa Lyon Ufaransa , kuliko na makao makuu ya Interpol kwenda China mnamo Septemba 25.

Interpol imesema imepokea barua ya kujiuzulu kwake mara moja kutoka kwa ofisi ya rais.

Familia yake Meng haijawasiliana naye tangu andoke katika makao hayo makuu ya Interpol nchini Ufaransa

Gazeti la South China Morning Post lilikunuu taarifa zilizosema kuwa Bw Meng, 64, alipelekwa kwenda kuhojiwa nchini China.

Haijulikani ni kwani nini alikuwa anachunguzwa na mamlaka za nidhamu au alikuwa anazuiliwa wapi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *