Michuano ya Super Cup Kuendelea leo Singida United Vs Fc Leopard

Michuano ya Super Cup Kuendelea leo Singida United Vs Fc Leopard

1
942
0
Tuesday, 05 June 2018
Sports

Wachezaji wa FC Leopard wakipiga Jaramba

Kikosi cha Singida United Kikipiga Jaramba

Patashika Nguo Kuchanika nchini Kenya ambapo Michuano ya Super Cup Yanaendelea.

Leo Wawakilishi wengine wa Tanzania, Singida United itatupa karata yake ya kuwania kuingia nusu fainal itakapo kukutana na FC Leopard, ya Kenya kwenya michuano hiyo.

Jana tulishuhudia mnyama akitinga hatua ya Nusu fainal ya michuano hiyo baada ya kuwafunga timu ya Kariobang Sharks kwa penati 2-3.

Ratiba inaonesha Simba watakutana na Wababe wa Yanga, Kakamega Homeboyz kesho, na mshindi wa leo kati ya Singida United dhidi ya FC Leopard atakutana na Gori Mahia.

Na bingwa wa michuano hiyo atapata nafasi ya kwenda Uingereza kucheza na timu ya Evertoon inayoshiriki Ligi Kuu Uingereza.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *