Mizizi na asili ya nguli wa muziki duniani na visiwa vya Zanzibar

Mizizi na asili ya nguli wa muziki duniani na visiwa vya Zanzibar

Like
1006
0
Wednesday, 24 October 2018
Global News

Freddie Mercury

Filamu mpya imeingia sokoni kuhusu bendi ya mziki ya Queen kutoka Uingereza, na macho yameelekezwa tena juu ya maisha ya muimbaji kinara wa bendi hiyo Freddie Mercury.

Ushawishi wake jukwaani, mavazi, mizizi yake na kifo chake kutoana na maradhi yanayohusiana na ugonjwa wa ukimwi akiwa na umri wa miaka 45 mwaka 1991 ni kumbukumbu tosha za mwanamuziki huyo wa miondoko ya rock kuanzia miaka ya sabini na themanini.

Kile ambacho wengi hawakifahamu na hakizungumziwi sana katika filamu ni kuwa alizaliwa katika visiwa vya karafuu vya Zanzibar kwenye familia ambayo asili yake ni India na Uajemi.

Filamu hiyo mpya yajulikana kama Bohemian Rhapsody, the biography of Mercury.

Haya ni mambo mambo unastahili kuyafahamu kuhusu Freddie Mercury na Zanzibar.

Alizaliwa kama Farrokh Bulsara

Mercury alizaliwa katika hospitali ya serikali huko Zanzibar tarehe 5 Septemba mwaka 1946. Wazazi wake Bomi na Jer Bulasara wana mizizi yao huko Uajemi lakini walikuwa pia wameishi nchini India.

Nyumba familia ya Freddie Mercury walikuwa wanaishi Zanzibar

Boni Bulsara alitokea huko Bulsar Gujarat (ndio maana familia ina jina hilo) na kuhamia Zanzibar kufanya kazi kwenye mahakama kuu kama karani wa serikali ya Uingerezea.

Alimuoa Jer huko India na kumleta Zanzibar. Farrokh mtoto wao kifungua mimba alifuatwa miaka sita baadaye na binti yao, Karishma.

Mercury mara nyingi hakuongeza hadharani kuhusu malezi yake huko Zanzibar.

Waliishi kwenye nyumba nzuri iliyokuwa ikiangalia baharini kwenye mji wa Stone Town ambayo ni sehemu ya kihistoria ya mji wa Zanzibar.

Leo hii mashabiki wake wanaweza kutembea sehemu alizokulia ikiwemo nyumbani kwake na mahakama ambapo baba yake alifanya kazi. Pia kuna mgahawa uitwao Mercury’s.

Nyumba ya familia ya Freddie Mercury huko Stone Town

Farrokh Bulsara alikulia kwenye mitaa ya Stone Town

Suala tata kwa Wazinzibari wengi na wafuasi wa dini ya Zoroastria ambayo Mercury alikuwa mfuasi ni kuwa mwanamuziki huyo alikuwa ni shoga. Uislam ndio dini yenye wafuasi wengi Zanzibar na ngono ya jinsia moja iliharamishwa kisheria na kufanywa kosa la jinai mwaka 2004.

Mwaka 2006, kundi moja la Wiaslamu lilizua tafrani baada ya kuenea kwa fununu kuwa kundi la watalii mashoga lilipanga kuzuru Zanzibar kusherehekea miaka 60 ya kuzaliwa kwa nguli huyo.

Aligundua muziki akiwa mdogo

Miaka ya kwanza ya masomo ya Mercury ni katika shule ya Wamishenari huko Zanzibar ambapo alifunzwa wa watawa wa Kianglikana. Lakini akiwa na umri wa miaka minane wazazi wake waliamua kumpleka shuleni huko India.

Freddie Mercury (wa pili kushoto) na bendi ya Queen mwanzo wa miaka ya sabini

Alisomea shule ya St Peter’s Church of England huko Panchgani kusini mashariki mwa mji wa Bombay (sasa Mumbai).

Wakati akiishi na shangazi na mababu zake huko Bombay ndipo akagundua kuwa aliupenda muziki. Pia aliunda bendi yake ya kwanza ya Hectics.

Familia yake ilikimbia mapinduzi

Freddie alirejea kutoka Zanzibar 1963, mwaka ambao visiwa hivyo vilipata uhuru kutoka Uingereza na kumalizia masomo katika shule ya Kikatoliki ya St Joseph’s Convent School.

Rafiki yake mmoja kutoka nyakati hizo anakumbuka jinsi walikuwa wakiogelea baharini baada ya kutoka shuleni na pia walivyokuwa wakiendesha baiskeli ufukweni sehemu za kusini.

Ramani

Lakini nyakati nzuri zilikuwa fupi. Mwaka 1964 mapinduzi yaliwatimua Waarabu waliokuwa wanatawala ambapo yakisiwa watu 17,000 waliuawa.

Jamhuri ikaundwa na marais wa Zanzibar na Tanganyika, kwa kusaini mkataba wa umoja. Wakaunda Jamhuri ya Muungano Tanzania.

Famialia ya Bulsara na wengine wengi wakakimbia visiwa hivyo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *