MLIPUKO WAUA 70 LIBYA

MLIPUKO WAUA 70 LIBYA

Like
212
0
Friday, 08 January 2016
Global News

WATU  70 wameuwawa  wakati  lori lililokuwa limewekewa  miripuko  kuripuka  katika  kambi  ya  polisi Kaskazini  Magharibi  ya  Libya  katika  mji  wa  pwani  wa Zliten.

 

Watu  wengi  wamejeruhiwa  katika  shambulio hilo  la  kujitoa  muhanga, ambalo  lilishambulia kundi  la maafisa  wa  polisi  waliokuwa  wamekusanyika  jana katika kambi .

 

Kwa  mujibu  wa  watu  walioshuhudia,  lori  hilo  lililokuwa na  miripuko  liligonga  katika  lango  la  kambi  hiyo ambayo  inatumiwa  kuwapa  mafunzo  walinzi  wa  pwani.

Comments are closed.