SAMATTA ATWAA TUZO YA MWANASOKA BORA AFRIKA LIGI ZA NDANI

SAMATTA ATWAA TUZO YA MWANASOKA BORA AFRIKA LIGI ZA NDANI

Like
234
0
Friday, 08 January 2016
Slider

Nyota ya Tanzania inayowika TP Mazembe ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Mbwana Ally Samatta amenyakua tuzo ya mwanasoka bora wa Afrika anachezea ndani ya bara la Afrika.

 

Tuzo ya mwanasoka bora barani Afrika imemwendea Pierre-Emerick raia wa Gabon anayesakata kambumbu katika klabu ya Borussia Dotmund nchini Ujerumani.

Tuzo hizo za kila mwaka zinazotolewa na Shirikisho la soka barani Afrika almaarufu kama CAF zimetolewa usiku wa kuamkia Ijumaa mjini Abuja nchini Nigeria.

Timu bora kwa wanaume kwa mwaka uliopita ni kutoka Ivory Coast.

Kwa upande wa timu ya wanawake ya mwaka tuzo imekwenda kwa timu ya Cameroon

 

Kocha bora wa mwaka ni – Herve Renard, kutoka Ivory Coast, tuzo ambayo ameishinda kwa mwaka wa pili mfululizo.

Klabu bora ya soka barani Afrika ni TP Mazembe, kutoka DR Congo

Mwanasoka bora wa kike Afrika ni Gaelle Enganamouit kutoka Cameroon

Mwamuzi bora wa mwaka ni Bakary Gassama kutoka nchini Gambia

Tuzo hizo zilipambwa na shamra shamra za kila aina kutoka kwa wasanii maarufu pamoja na wanenguaji walitumbuiza akiwemo mwanamuziki nguli kutoka nchini Mali, Salif Keita pamoja na mwanamuziki kutoka Nigeria Omowumi.

 

Comments are closed.