mo dewji apatikana usiku wa manane

mo dewji apatikana usiku wa manane

Like
748
0
Saturday, 20 October 2018
Local News

Afisa mkuu wa polisi wa kanda ya Dar es salaam Lazaro Mombasa aliyetembelea nyumbani kwao Dewji kuthibitisha kurejea kwake nyumbani, watu waliomkamata walikuwa na lafudhi ya mojawapo ya lugha za mataifa ya Afrika Kusini. Aliongezea kwamba hatua hiyo imethibitisha wazi kwamba waliomteka sio watanzania.

Mo Dewji; Ninawashukuru Watanzania kwa kuniombea

”Nataka kuuthibitishia umma wa Tanzania kwamba nimefika nyumbani kwa akina Mo Dewji nimeongea naye niko na kikosi cha makachero hapa na ndugu yetu ni mzima kama IGP alivyozungumza na umma kwamba jeshi la polisi litaendelea na uchunguzi ili kuhakikisha kwamba tunampata muhusika akiwa mzima.

Mo Dewji ambaye alionekana mchovu alimshukuru mwenyezi mungu na serikali ya rais Pombe Magufuli pamoja na Watanzania kwa kumuombea.

”Namshkuru mwenyezi mungu , serikali ya magufuli na IGP , ahsanteni mimi ni mzima nawashukuru Watanzania wote kwa kuniombea.

Babake Mo alivimbia vyombo vya habari kwamba mwendo wa saa nane alifajiri walipokea simu ya Mo kwamba yuko salama na moja kwa moja wakaelekea katika eneo la Gymkhana ambako alikuwa amewachwa na watekaji wake.

” Tumshukuru mwenyezi Mungu kwamba tumempata salama na anaendelea vizuri. Walikuwa wamemuacha pale na kuondoka. Lakini alikuwa hajafungwa na yuko sawasawa. Tunawashukuru Watanzania wote na rais”.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *