Mpambe wa Rais Magufuli aombwa apangiwe kazi nyingine

Mpambe wa Rais Magufuli aombwa apangiwe kazi nyingine

1
855
0
Thursday, 12 April 2018
Local News

Mkuu wa Majeshi ya Tanzania, Venance Mobeyo, amemuomba Rais Magufuli aridhie mpambe wa Rais wake, Kanali MN Nkelemi kupangiwa kazi nyingine baada ya kupandishwa cheo kutoka Kanali, kuwa Brigedia Jenerali.

 

Hata hivyo amesema kuwa “Pamoja na upandishwaji vyeo huo nimeomba pia aridhie na amekubali kupandishwa cheo Luteni Kanali DPM Mulunga kuwa Kanali na kwa cheo hicho Mh. Rais ameridhia vilevile ateuliwe kuwa mpambe wa Rais kuanzia leo taratibu zingine za kuwavisha vyeo hivyo zitafanyika kesho Makao Makuu ya Jeshi ,” amesema Mobeyo.

 

Comments are closed.