Msafara wa Rais Magufuli wapata ajali Mara

Msafara wa Rais Magufuli wapata ajali Mara

Like
604
0
Wednesday, 05 September 2018
Local News

MSAFARA wa Rais John Magufuli uliokuwa ukielekea wilayani Ukerewe mkoani Mwanza, umepata ajali katika kijiji cha Kasuguti, kata ya Kisorya, wilayani Bunda mkoani Mara, leo Septemba 4, 2018 baada ya magari manne kugongana katika eneo ambalo barabara ilikuwa ikijengwa.
Taarifa za awali zinadai kuwa waandishi wawili wa habari wamejeruhiwa baada ya gari walimokuwa kupinduka.
Amesema chanzo cha ajali hiyo ni vumbi lilikuwa limetapakaa barabarani kutokana na msafara huo hivyo madereva kushindwa kuona vizuri njia lakini hakuna madhara makubwa licha ya gari moja kubondeka ubavuni baada ya kupinduka.
Majeruhi wa ajli hiyo ni watu wawili ambao ni Neema Emmanuel, waandishi wa Gazeti la Nipashe ambaye ameumia kichwani na Tunu Heriman ambaye alipata mshituko tu lakini kwa sasa wote wanaendelea vizuri

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *