MUGABE ASISITIZA KUTOACHIA MADARAKA

MUGABE ASISITIZA KUTOACHIA MADARAKA

Like
269
0
Thursday, 26 May 2016
Global News

RAIS wa Zimbabwe Robert Mugabe amesema kuwa yeye sio Mmarekani wala Muingereza wakati akiwahutubia karibu watu elfu 50,000, wafuasi wake kwenye mkutano uliofanyika kwenye mji mkuu Harare kwa heshima yake.

 

Mugabe mwenye umri wa miaka 92 amekana uwezekano wowote wa kuondoka madarakani na kuwashambulia viongozi hasimu ndani ya chama tawala cha ZANU-PAFU kwa kupanga kumrithi.

 

Amesema kuwa yeye anawahudumia watu wa Zimbabwe na kuwa ataondoka tu ikiwa watu wangetaka afanye hivyo.

Comments are closed.