Muungano wa Afrika umeiomba DR Congo uahirishe kutangaza matokeo kamili ya uchaguzi mkuu

Muungano wa Afrika umeiomba DR Congo uahirishe kutangaza matokeo kamili ya uchaguzi mkuu

Like
459
0
Friday, 18 January 2019
Global News

Muungano wa Afrika (AU) umeitaka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo iahirishe kutangaza matokeo ya uchaguzi mkuu.

Muungano huo unaonuia kuhimiza umoja na demokrasia, unasema una “shaka kubwa” na matokeo ya awali yaliotangazwa wiki iliyopita.

Matokeo hayo yalimpa ushindi mgombea wa upinzani Felix Tshisekedi lakini mpinzani wa utawala uliopo.

Matokeo ya mwisho yanatarajiwa kutangazwa leo Ijumaa.

Kumezushwa maswali mengi kuhusu uhakika wa matokeo hayo huku kukiwepo shutuma kwamba Tshisekedi anapanga mpango wa kugawana madaraka na rais anayeondoka Joseph Kabila.

Baadhi ya viongozi katika Muungano wa Afrika na serikali walikutana katika mji mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa jana Alhamisi na kutoa tamko kuhusu uchaguzi huo wa Desemba 30 unaopingwa pakubwa.

“Kumekuwa na shaka kubwa kuhusu namna matokeo ya awali yalivyokusanywa, kama ilivyotangazwa na tume huru ya kitaifa ya uchaguzi kwa kura zilizopigwa,” taarifa ya muungano huo imesema.

“Kadhalika, AU imetaka kuahirishwa kutangazwa kwa matokeo ya mwisho ya uchaguzi mkuu huo,” iliongeza taarifa.

Fayulu anatuhumu kwamba mshindi wa muda bwana Tshisekedi alikubaliana na rais anayeondoka Joseph Kabila.

Kabila amehudumu kwa miaka 18 na matokeo, iwapo yatathibitishwa, yataidhinisha ukabidhi wa kwanza wa uongozi kwa mpangilio tangu taifa hilo lipate uhuru kutoka kwa Ubelgiji mnamo 1960.

Tume ya uchaguzi imesema Tshisekedi alishinda 38.5% ya kura, ikilinganishwa na 34.7% alizoshinda Fayulu. Mgombea wa muungano wa serikali Emmanuel Shadary alijizolea 23.8%.

Fayulu aliwasilisha kesi katika mahakama ya katiba kupinga matokeo hayo Jumamosi akitaka

Matokeo hayo yanatarajiwa kutangazwa kama ni mapema sana leo, na wataalamu wanasema kuna uwezekano wa matokeo matatu.

Huenda mahakama:

  • Ikathibitisha ushindi wa Tshisekedi
  • Ikaagiza kura kuhesabiwa upya
  • Ikafutilia mbali matokeo yote na kuitisha uchaguzi mpya

Lakini mahakama haijawahi kubatilisha matokeo katika siku za nyuma.

Kumekuwa na hisia gani?

Kutangazwa kwa Tshisekedi mshindi kumepingwa pia na kanisa katoliki lenye ushawishi mkubwa na ambalo pia linasema liliwatuma waangalizi 40,000 wa uchaguzi kote nchini.

Wataalamu waliopo katika serikali nchini Marekani, Ufaransa na Ujerumani pia wametilia shaka matokeo hayo.

“Duru za kuaminika” zinaeleza mapigano kati ya jamii za Banunu na Batende yalizuka katika vijiji vinne huko Yumbi, ofisi ya Umoja wa mataifa kuhusu haki za binaadamu inasema.

Idadi kubwa ya wakaazi wa eneo hilo inaarifiwa wameachwa bila ya makaazi.

Uchaguzi mkuu wa Desemba 30 uliahirishwa huko Yumbi kutokana na ghasia.

Raia walioachwa bila ya makaazi ni pamoja na watu 16,000 waliotafuta hifadhi kwa kuvuka mto Congo hadi katika nchi jirani ya Congo-Brazzaville, umeongeza.

Nyumba 465 na majengo yaliteketezwa au kuharibiwa, zikiwemo shule mbili za msingi, kituo cha afya, soko na ofisi ya tume huru ya uchaguzi katika eneo hilo, Umoja huo umesema.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *