PROF. MSERU ATAMBULISHWA RASMI KUWA MKURUGENZI WA BODI YA HOSPITALI YA MUHIMBILI

PROF. MSERU ATAMBULISHWA RASMI KUWA MKURUGENZI WA BODI YA HOSPITALI YA MUHIMBILI

Like
640
0
Thursday, 12 November 2015
Local News

HOSPITALI ya Taifa ya Muhimbili leo imempokea na kumtambulisha rasmi mkurugenzi mpya wa bodi ya hospitali hiyo Profesa Lawrence Mseru kufuatia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania dokta John Pombe Magufuli kuivunja bodi iliyokuwa ikiongozwa na mkurugenzi dokta Hussein Kidanto siku chache zilizopita.

 

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar Salam Afisa uhusino wa hospitali hiyo dokta Amnieli Eligisha amesema kuwa tayari mkurugenzi huyo ameanza kazi ya kuhakikisha ana boresha huduma ya matibabu ikiwemo kufanyia matengenezo mashine zote zikiwemo SITI SCAN kwa kufuata Agizo lililotolewa na Rais.

 

ELIGESHA ameongeza kuwa upande wa tatizo la mashine MRI limeshughulikiwa na tayari imeanza kufanya kazi kama inavyotakiwa huku mashine za Siti Scan zimeshaanza hatua za awali ili za kufanyiwa matengenezo.

Comments are closed.