WAFANYAKAZI URAFIKI WAGOMA KUSHINIKIZA NYONGEZA YA MISHAHARA

WAFANYAKAZI URAFIKI WAGOMA KUSHINIKIZA NYONGEZA YA MISHAHARA

Like
296
0
Thursday, 12 November 2015
Local News

WAFANYA KAZI wa kiwanda cha nguo cha urafiki kilichopo mabibo Jijini Dar es salaam leo wamegoma kufanyakazi kwa kushinikiza uongozi wa kiwanda hicho kuwaongezea mishahara yao pamoja na kulipwa malimbikizo mengine wanayodai.

 

Wakizungumza na Efm wafanyakazi hao wamesema kuwa mishahara wanayo lipwa ni kidogo sanjari na makato mengine kwenye mishahara yao ikiwemo bima ya Afya ingawa Awali walishafungua kesi mahakama kuu ya rufaa ili waweze kulipwa madeni yao lakini bado hawajalipwa hadi sasa.

Kwa upande wake Naibu meneja mkuu msaidizi wa kiwanda hicho Moses Swai amekiri kuwepo kwa madai hayo na kwamba waliunda timu ya kuchambua madai hayo kulinganan na taratibu na kufanya mkutano wa pamoja na chama cha wafanyakazi-TUICO.

Comments are closed.